1.1.1 Leba ya kawaida

Leba ya kawaida huwa na viashirio hivi:

  • Kuanza kighafla. (Leba ya kawaidahuanza kivyake bila usaidizi wowote wa kimatibabu)
  • Mikazo ya uterasi huwa yenye utaratibu na mpangilio maalum.
  • Mtoto kutanguliza utosi. (Utosi wa mtoto hutanguliza kupitia kwenye uwazi wa seviksi, kama vile ulivyojifunza katika Kipindi cha 6 cha moduli ya Utunzaji Katika Ujauzito.
  • Kuzaa kupitia uke hufanyika bila usaidizi wa kitaalam kwa muda wa chini ya saa 18 kwa mwanamke anayezaa kwa mara ya kwanza (mwanamke primigravida). Kwa mwanamke anayejifungua kwa mara ya pili (au zaidi) (maltigravida), kuzaa kupitia uke hutokea bila usaidizi zaidi wa kitaalam kwa muda wa chini ya saa 12.
  • Hakuna matatizo kwa mama ama fetasi.

Leba yoyote inayohitilafiana na viashirio hivi si ya kawaida. Leba isiyo ya kawaida huitaji kushughulikiwa na mtaalam. Vipindi vya 8 -11 vinaelezea jinsi ya kushugulikia aina mbalimbali za leba isiyo ya kawaida. Baadaye, utajifunza kuhusu dalili zinazokuashiria wewe na mama kuwa leba halisi imeanza.

1.1 Asilia isiyodhahiri ya leba

1.2 Utajuaje kuwa leba halisi imeanza?