1.2.1 Mikazo tosha ya uterasi ni nini?

Wakati wa leba halisi, mikazo tosha ya uterasi hutokea. Mikazo ya uterasi hutathminiwa kwa kuzingatia viashirio vitatu: idadi ya marudio, muda inayochukua na makali ya mikazo:

  • Idadi ya marudio ya mikazo ya uterasi ni mara 3-4 kila dakika 10.
  • Kila mkazo huchukua sekunde 40-60, ambazo huitwa muda wa mikazo.
  • Mwanamke anasema kuwa anahisi mikazo ikiwa na kishindo. Kishindo hiki huitwa makali ya mikazo.

Ili kukadiria makali ya mikazo ya uterasi, chunguza kwa kupapasa fumbatio la mwanamke katika sehemu ya fandasi (juu) ya uterasi. (Kupapasa ni kugusa kwa mikono yako ili kuhisi). Unaweza kupapasa sehemu za fetasi kati ya vipindi vya mikazo uterasi unapotulia na misuli ya pembezoni mwa uterasi imelainika. Hata hivyo, mikazo mikali inapoanza, pembezoni mwa fumbatio juu ya uterasi hukazana hivyo hautaweza kuhisi viungo vya fetasi kwa kupapasa. Ukifinya kwa nguvu ukitumia vidole, mama huhisi uchungu.

Katika Kipindi cha 4 ulijifunza jinsi ya kurekodi marudio, muda na makali ya mikazo kwenye chati iitwayo

1.2 Utajuaje kuwa leba halisi imeanza?

1.2.2 Damu tetelezi na kuvuja kwa kiowevu cha amnioni