1.2.3 Tofautisha kati ya leba halisi na leba bandia

Hali inayojulikana kama leba bandia inaweza kutokea wiki moja au mbili kabla ya leba ya kweli. Wakati wa leba bandia, mwanamke huhisi mikazo isiyo na utaratibu na iliyo na uchungu kiasi kidogo kuliko wa wakati wa leba ya kweli. Kwa kawaida, mikazo hii haiendelei. Jedwali1. 1 inalinganisha viashirio vya leba ya kweli na ile bandia. Mwanamke anapokuwa na leba bandia, mhimize asife moyo. Mweleze kuwa ingawa angali hajapata leba halisi, dalili hizi zinaonyesha kuwa itaanza hivi karibuni. Mshauri kuhusu dalili za leba halisi. Mueleze akuite au aje katika Kituo cha Afya punde dalili za leba halisi zikijitokeza. Dalili za leba halisi zimeelezwa katika jedwali 1.1 na Kipindi kinachofuata.

Jedwali 1.1 Viashirio vya leba halisi na bandia
ViashirioLeba ya kweliLeba ya bandia
Mikazo ya uterasiMikazo hutokea ikifuata utaratibu maalum lakini muda baina ya kila mkazo hupungua polepole.Mikazo hutokea bila kufuata utaratibu wowote.
MudaMuda wa kila mkazo huongezeka polepole. Muda haubadiliki, aidha kuwa mrefu au mfupi
MikazoMikazo huongezeka kwa nguvu na kasi. Mikazo haiongezeki kwa vyovyote.
Kupanuka kwa seviksiSeviksi huendelea kupanuka. Seviksi haipanuki, hubaki chini ya sentimita 2.
MaumivuMaumivu ya mgongo, ambayo hayatulizwi kwa dawa zenye nguvu ya kutuliza maumivu makali. Maumivu hayapo katika mahali popote mahususi na kawaida hutulizwa kwa dawa za kutuliza maumivu ama kwa kutembea.

1.2.2 Damu tetelezi na kuvuja kwa kiowevu cha amnioni

1.2.4 Kumsaidia mama kutambua leba halisi