1.2.4 Kumsaidia mama kutambua leba halisi

Hakuna anayeweza kujua wakati leba itaanza. Hata hivyo, baadhi ya dalili huashiria kwamba itaanza punde. Mara nyingi, watoto hushuka chini ya fumbatio takriban wiki mbili kabla ya kuzaliwa, hali inayojulikana kama kusahaulika. Kwa kawaida, mwanamke atahisi kuwa mtoto “haelei” kwenye fumbatio, na hasukumi juu tumbo la mama. Ikiwa mwanamke aliwahi kuzaa, huyu mtoto huenda asishuke hadi wakati wa kuanza kwa leba.

Dalili nyingine zinaweza kuanza siku moja au mbili tu kabla ya kuanza kwa leba. Kinyesi cha mama kinaweza kubadilika ama kiasi kidogo cha damu tetelezi (damu iliyochanganyika na utetelezi) kinaweza kutoka kwenye uke. Wakati mwingine, mfuko wa maji hupasuka kabla ya leba kuanza.

Kutambua leba halisi si jambo rahisi kwa mama, hasa kama mimba hii ni ya kwanza. Anaweza kukuita au kuja kwenye kituo cha afya mara nyingi akifikiria kuwa maumivu madogo ni mwanzo wa leba halisi. Kumshauri mama na jamii yake kuhusu kujitayarisha kuzaa ni sehemu ya lengo la utunzaji kabla ya kuzaa. (Kipindi cha 13 cha Somo cha moduli ya Utunzaji wa kabla ya Kuzaa). Unapomfunza jinsi ya kutambua dalili za leba halisi na awamu anazohitaji kuchukua, tumia lugha anayoweza kuelewa. Mweleze bayana kuhusu jinsi atakavyohisi kwenye fumbatio lake. Wajibu wako ni muhimu. Unasaidia kupunguza wasiwasi wa mama kuhusu leba. Unaweza pia kumsaidia kupunguza gharama na muda anaopoteza anapotembelea kituo cha afya kwa sababu ya leba bandia au maumivu madogo.

Mweleze viashirio hivi vya leba halisi:

  • Uchungu wa kusukuma chini unaongezeka pindi wakati unavyoendelea. Uchungu huu hutokea mara 3-5 kila dakika 10. (Hakikisha kama anafahamu au anaweza kukadiria muda wa dakika 10).
  • Kwa kawaida mwanamke huhisi uchungu unaosukuma chini, kwanza katika sehemu ya chini ya mgongo. Uchungu huu huzunguka hadi katika sehemu ya chini ya fumbatio chini ya kitovu.

Mweleze mambo haya kwa kutumia fumbatio lake:

  • Kitakachotokea kwa sababu ya kusahaulika.
  • Sehemu atakayohisi ugumu kwenye fumbatio wakati wa mikazo.
  • Sehemu atakayohisi uchungu zaidi unaosukuma chini.

1.2.3 Tofautisha kati ya leba halisi na leba bandia

1.3 Awamu za leba