1.3.2 Awamu ya pili ya leba
Awamu ya pili ya leba huanza wakati seviksi imepanuka kabisa (sentimita 10) na kuisha mtoto anapozaliwa. Baada ya seviksi kupanuka kabisa, mama kawaida hupata hisia za kutaka kusukuma. Mama akisukuma kulingana na mikazo ya uterusi, mtoto huteremkia kwenye seviksi na kushukia ukeni. Mwendo huu wa mtoto hujulikana kama kushuka kwa fetasi. Kiwango cha kushuka kwa fetasi ni kiashirio muhimu cha jinsi leba inavyoendelea. Habari hii imeelezwa kwa kina hapo baadaye. Muda wa awamu ya pili ni wastani wa masaa 1-2. Jedwali 1.2 inaeleza kwa muhtasari ishara na dalili za awamu ya kwanza na ya pili ya leba ya kawaida.
Dalili na ishara | Awamu | Awamu |
---|---|---|
Seviksi haijapanuka | Leba bandia, mwanamke hayuko katika leba | |
Mikazo ya uterasi isiyo taratibu wala mikali | Leba bandia, mwanamke hayuko katika leba | |
Mikazo ya uterasi iliyo taratibu lakini isiyo mikali | Ya kwanza | Fiche |
Seviksi imepanuka kiwango cha chini ya sentimita 4. Mikazo ni taratibu na mikali | ||
Seviksi imepanuka kwa sentimita 4-9 | ||
Kima cha kupanuka kawaida ni sentimita 1 kwa kila saa au zaidi | Ya kwanza | Wazi |
Fetasi inaanza kuteremka. Seviksi imepanuka kabisa (sentimita 10) | ||
Fetasi inaedelea kuteremka. | Ya pili | Ya vipindi vya mwanzo (haipelekei kuzaliwa) |
Mama hana hamu ya kusukuma. Seviksi imepanuka kabisa (sentimita 10) | ||
Sehemu tangulizi ya fetasi imefika sehemu ya chini ya pelvisi | Ya pili | Ya vipindi vya mwisho (inapelekea kuzaliwa) |
Mama hana hamu ya kusukuma |
Kuzaliwa kwa mtoto ni ishara ya mwisho wa awamu ya pili.
1.3.1 Awamu ya kwanza ya leba