1.3.4 Awamu ya nne ya leba

Saa 4 za kwanza punde baada ya plasenta kutoka huwa muhimu. Baadhi ya wataalam wamekipa kipindi hiki jina awamu ya nne ya leba. Mwanamke anaweza kuvuja damu kwa wingi baada ya plasenta kutoka. Hii hutokea iwapo mikazo ya uterasi inasababisha kutofungika kwa mishipa ya damu iliyofunguka kufuatia kubanduka kwa plasenta kwenye pembezoni mwa uterasi. Kwa hivyo, unafaa uwe makini ili kutambua na kuthibiti damu inayovuja baada ya kuzaa. Damu hii inaweza kuwa dhahiri au iliyofichika. (Utajifunza zaidi kuhusu kuvuja damu baada ya kuzaa katika Kipindi cha 11 cha Somo kwenye moduli hii. )

Chunguza plasenta, membreni na kodo. Hakikisha kuwa vyote hivi ni vizima na vya kawaida (Kipindi cha 6). Rekodi kiwango cha shinikizo la damu na mpwito wa mishipa ya mama baada ya kuzaa na kila baada ya dakika 15 kwa saa 4 za kwanza. Kwa kawaida, baada ya plasenta kutoka, uterasi huwa ngumu kwa sababu inaendelea kukazika. Mwanamke anaweza kuhisi mikazo mikali baada ya kuzaa. Mwakikishie kuwa mikazo hii ni salama na kwamba inaweza kusaidia kusitisha kuvuja kwa damu.

1.3.3 Awamu ya tatu ya leba

1.4 Utaratibu wa leba ya kawaida