1.4.1 Kufungamana
Kufungamana ni utaratibu ambapo kichwa cha fetasi huingia kwenye uwazi wa pelvisi. (Mchoro 1.3, mchoro wa 2). Kipenyo cha parietombili ni kipimo kutoka ncha moja ya sikio hadi nyingine kupitia juu ya utosi wa mtoto (Mchoro 1.4). Kichwa hufungamana wakati kipenyo cha parieto mbili hushuka kwenye uwazi wa pelvisi, nacho kisogo kipo katika upeo wa mifupa ya iskiamu katika pelvisi ya mama (Mchoro 1.5).
1.4 Utaratibu wa leba ya kawaida