1.4.2 Kushuka

Kushuka ni mwendo endelevu wa chini wa mtoto ambapo sehemu (kwa kawida kichwa) hutokezea kupitia pelvisi. Ni sharti mikazo ya uterasi iwe dhabiti na itokee kwa utaratibu maalum. Ni sharti kichwa cha mtoto na nafasi ya pelvisi ya mama vitoshane kwa ukubwa ili mtoto aweze kupitia. Mtoto huendelea kushuka kwenye nafasi ya ndani ya pelvisi.

Nafasi ya pelvisi imezungukwa na mifupa ya pelvisi. Uterasi inaposukumika chini kwa kishindo, mifupa ya skalpu ya mtoto hupishana mara kwa mara katika mistari ya sucha. Hii hufanyika ili kichwa kipitie kwenye nafasi hii ndogo. Utaratibu huu wa kupishana hujulikana kama kufinyangika. Aina za kufinyangika zinazofanyika mara nyingi ni:

  • Mojawapo ya mifupa ya parieto hupishana na ule mwingine kwenye sucha ya sajita. (Mchoro 1.4)
  • Mfupa wa kisogo hupishana na wa panja.
  • Mfupa wa mbele hupishana na mifupa ya parieto.

1.4.3 Kukunjika