Muhtasari wa Kipindi cha somo la 1

Katika Kipindi cha somo la 1, ulijifunza yafuatayo:

  1. Leba halisi ni utaratibu asilia. Wakati wa leba, mikazo ya uterasi hutokea kwa utaratibu maalum, yenye kutabirika na mikali. Mikazo huendelea kuongezeka taratibu na kusababisha seviksi kufitika na kupanuka.
  2. Leba halisi inaweza kuanza bila damu tetelezi au maji kuvunjika (kupasuka kwa membreni za fetasi).
  3. Mwanamke aliye na leba bandia huwa na mikazo ya uterasi isiyo taratibu. Dawa za kutuliza maumivu zinazoweza kupunguza makali ya mikazo hii.
  4. Mwanamke mwenyewe anaweza kutambua akiwa katika leba ya kweli. Wakati wa leba, uchungu unaotokana na kusukuma chini hutokea mara 3-5 kila baada ya dakika 10, na kila mkazo huchukua sekunde 40-60.
  5. Kuna awamu nne za leba:
    • Awamu ya kwanza huanzia na leba halisi na kukamilika seviksi ikipanuka kabisa (sentimita 10). Awamu hii ina awamu fiche na wazi.
    • Awamu ya pili huanza wakati seviksi imepanuka kabisa na kuisha mtoto anapozaliwa.
    • Awamu ya tatu huanza mtoto anapozaliwa na kukamilika plasenta inapotoka.
    • Awamu ya nne ni masaa 4 ya kwanza baada ya plasenta kutoka. Katika awamu hii, mtazame mama kwa makini kama ufanyavyo wakati wa leba na kuzaa.
  6. Katika leba inayoendelea kwa kawaida, mtoto hufanya miendo saba mikuu huku akishuka chini kwenye njia ya uzazi: kufungamana, kushuka, kukunjika, kuzungukia ndani, kutandazika, kuzungukia nje (kurejea), na kutolewa.
  7. Fetasi hushuka kila wakati wa kila mwendo.
  8. Fuvu la kichwa cha mtoto linaweza kufinyangika linapopitia kwenye pelvisi ya mama. Nguvu ziletwazo na mikazo inayomsukuma kupita kwenye nafasi nyembamba inaweza kufinyanga fuvu la kichwa cha mtoto.

Maswali ya Kujitathmini (MK) ya Kipindi cha Somo la 1