Maswali ya Kujitathmini (MK) ya Kipindi cha Somo la 1

Kwa vile umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali haya ili kutathmini jinsi ulivyofanikiwa katika malengo ya Somo la Kipindi hiki. Andika majibu yako katika shajara yako ya masomo na uyajadili na mkufunzi wako katika Mkutano Saidizi wa Somo unaofuata. Linganisha majibu yako na maandishi ya kukumbuka yaliyo katika Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa moduli hii.

MK 1.1 (linatathmini Malengo ya Somo 1.1)

Andika kwenye kijikaratasi kila mojawapo ya maneno yaliyoandikwa kwa herufi nzito yaliyoorodheshwa hapa. Kunja kila kijikaratasi kisha ukitumbukize kwenye kikapu au bakuli.

Chukua kila kijikaratasi kimoja baada ya kingine kisha ujaribu kufasili kila neno. Andika majibu yako kwenye Shajara yako ya Masomo. Mwisho, linganisha majibu yako na fasili iliyo kwenye Kipindi hiki cha somo. Rudia zoezi hili hadi uyafahamu maneno yote: leba halisi, kuvutika juu na kupanuka kwa seviksi baada ya kila mkazo, kupanuka, sehemu iliyotangulia, damu tetelezi, kupasuka kwa membreni, kufungamana, kushuka, awamu ya kwanza, awamu ya pili, awamu ya tatu, awamu ya nne

Answer

Angalia fasili yako ya maneno yaliyoandikwa kwa herufi nzito. Angalia kila neno katika Kipindi cha 1 cha Somo kisha ulinganishe uliyoyaandika kwenye Shajara yako ya Masomo na fasili iliyo katika Kipindi hiki. Iwapo kuna fasili yako yoyote ambayo haikulingana, jaribu Zoezi 1.1 tena hadi uyapate kwa usahihi.

Mwisho wa jibu

Soma Kauli ya Somo 1.1 kisha ujibu maswali yanayoifuata.

Kauli ya Somo 1.1 Bi. Abeba

Bi Abeba ana umri wa miaka 30 na anazaa mtoto wake wa kwanza. Ametembelea kituo cha afya kwa sababu masaa matatu yaliyopita alianza kuhisi uchungu wa kila mara unaosukuma kwenda chini. Anaeleza kuwa uchungu huu unaanzia mgongoni na kusonga hadi sehemu ya mbele ya fumbatio. Anaeleza kuwa kila mara, uchungu unadumu kwa takriban sekunde 40, na kuwa unatokea mara 2-3 baada ya kila dakika 8. Baada ya kumchunguza, unatambua kuwa seviksi yake imefitika na kupanuka kabisa na kwamba kipenyo chake kina upana wa sentimita 4. Mama mkwe wa Bi Abeba alimwambia kuwa leba haijaanza kwa sababu “damu tetelezi” ingali haijatoka.

MK 1.2 (linatathmini Malengo ya Masomo 1.2 na 1.3)

  1. Ni dalili zipi, kulingana na maelezo ya Bi. Abeba, zinazoonyesha kuwa yuko katika leba ya kweli?
  2. Je, amefika awamu ipi ya leba na umetambua vipi?
  3. Utamwambia nini Bi. Abeba ili atambue kwamba yuko katika leba halisi?

Answer

  1. Bi. Abeba yuko katika leba halisi kwa sababu uchungu wake ni dalili ya mikazo tosha ya uterasi. Mikazo inatokea kila mara (mara 2-3 kila baada ya dakika 8), na muda inayochukua ni sekunde 40, jambo ambalo linatarajiwa katika leba halisi. Seviksi yake imevutika na kupanuka kwa sentimita 4 baada ya saa 3 za mikazo kutokea.
  2. Yeye yuko katika awamu ya kwanza ya leba. Yeye yuko kati ya awamu fiche na iliyo wazi, ambayo hutokea wakati seviksi imepanuka hadi sentimita 4.
  3. Mhakikishie Bi. Abeba kwamba leba inaweza kuanza hata kabla ya damu tetelezi kuvuja. Mikazo yake imekuwa ikija kwa saa 3 bila kusita. Makali na utaratibu wa kikazo hii ni kama inavyotarajiwa katika leba ya kawaida.

Mwisho wa jibu

MK 1.3 (linatathmini Malengo ya Somo 1.2)

Jedwali 1.3 linaorodhesha tofauti baina ya leba halisi na bandia. Jaza mapengo haya kwa maelezo yafaayo.

Jedwali 1.3 Leba halisi na bandia
Leba halisiLeba bandia
Mikazo hutokea kwa nyakati zinazoweza kutabirika
Muda unaochukua kila mkazo huongezeka pole pole
Makali ya mikazo hayabadiliki
Seviksi huendelea kupanuka
Maumivu huondolewa kwa kutembea au na matibabu ya kuyapunguza.

Answer

Toleo lililojazwa la Jedwali 1.3 limeonyeshwa hapa.

Leba halisiLeba bandia
Mikazo hutokea kwa nyakati zinazoweza kutabirikaMikazo hutokea kwa nyakati zisizoweza kutabirika.
Muda unaochukua kila mkazo huongezeka pole pole Muda haubadiliki: iwapo ni mrefu au mfupi
Makali ya mikazo huzidiMakali ya mikazo hayabadiliki
Seviksi huendelea kupanukaSeviksi haipanuki
Maumivu hayatulizwi kwa matibabu ya kutuliza maumivuMaumivu huondolewa kwa kutembea au matibabu ya kuyapunguza.

Mwisho wa jibu

MK 1.4 (linatathmini Malengo ya Masomo 1.1, 1.4 na 1. 5)

Ni elezo lipi lisilo la kweli? Katika kila kauli, eleza lisilo la kweli.

  • A.Wepesi ni utaratibu ambapo mtoto huelea kwenye fumbatio muda mfupi kabla ya leba kuanza.
  • B.Awamu ya pili ya leba huisha mtoto anapotoka kwenye njia ya uzazi.
  • C.Awamu ya nne ya leba hudumu kwa saa 4 na kuanza punde plasenta na membreni zinapotolewa.
  • D.Kupishana kwa mifupa ya fuvu la kichwa cha mtoto wakati wa kushukia kwenye pelvisi ya mama hujulikana kama kukunjika.
  • E.Kichwa cha mtoto hufungamana kisogo kinapofika katika upeo wa mifupa ya iskiamu katika pelvisi ya mama.
  • F.Wakati wa kuzaa kwa njia ya kawaida, mabega yote hutokeza kwa wakati mmoja.

Answer

  • A.si kweli. Wepesi ni utaratibu ambapo mtoto hushuka hadi sehemu ya chini ya fumbatio, muda mfupi kabla ya leba kuanza.
  • B.ni kweli. Awamu ya pili ya leba huisha mtoto anapotoka kwenye njia ya uzazi.
  • C.ni kweli. Awamu ya nne ya leba hudumu kwa saa 4 na kuanza punde plasenta na membreni zinapotolewa.
  • D.si kweli. Kupishana kwa mifupa ya fuvu la kichwa cha mtoto wakati wa kushukia kwenye pelvisi ya mama hujulikana kama kufinyangika (wala sio kutandazika).
  • E.ni kweli. Kichwa cha mtoto hufungamana wakati kisogo kipo katika upeo wa mifupa ya iskiamu.
  • F.si kweli. Wakati wa kuzaa kwa njia ya kawaida, bega moja la mtoto hutoka kwanza, kisha lile lingine kufuata.

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha somo la 1