Malengo ya Somo la Kipindi cha 2

Baada ya Kipindi hiki utakuwa na uwezo wa:

2.1 Kufasili na kutumia maneno muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (MK 2.5)

2.2 Kueleza jinsi ya kumchunguza kwa haraka mwanamke aliye katika leba. (MK 2.1)

2.3 Kueleza vipengele vya huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke wakati wa leba na kuzaa. (MK 2.3)

2.4 Kueleza jinsi ya kuchukua historia ya mwanamke aliye katika awamu ya kwanza ya leba ya kawaida. (MK 2.3)

2.5 Kueleza jinsi ya kupapasa fumbatio la mwanamke aliye katika leba ili kuchunguza ukubwa wa mtoto, hali na kutokezea kwake. (MK 2.2)

2.6 Kueleza jinsi ya kuchunguza uke wa mwanamke aliye katika leba ili kutathmini jinsi leba inavyoendelea. (MK 2.4)

2.7 Kutofautisha kati ya Malengo ya kawaida na yasiyo ya kawaida unapomchunguza mwanamke aliye katika leba. (MK 2.4)

Kipindi cha 2 cha Somo Kumchunguza Mwanamke aliye katika Leba

2.1 Mchunguze kwa haraka mwanamke aliye katika leba