2.1.1 Hatua za uchunguzi wa haraka

Unahitaji kukusanya:

  • Kadi yake ya huduma ya kabla ya kuzaa, ikiwa ulimhudumia hapo awali. Ikiwa ni mgeni kwako na tayari yuko katika leba, mwanzishie rekodi mpya ya afya.
  • Patografu ili kurekodi jinsi leba inavyoendelea. (Utajifunza jinsi ya kutumia patografu katika Kipindi cha 4.)
  • Glavu zilizotiwa dawa ya kuua vimelea.
  • Fetoskopu ya kusikiza jinsi moyo wa mtoto unavyodunda.
  • Themometa ya kupima kiwango cha joto la mama.
  • Saa au kipima muda kingine ili kisaidie kupima mdundo wa moyo wa fetasi na kiwango cha mpwito wa ateri za mama.
  • Sijafu ya kupimia shinikizo la damu kwa stethoskopu.
  • Swabu ya kusafisha msamba wa mwanamke kabla ya kumchunguza. [Tumia mipira 3-4 ya shashi iliyotiwa kwenye mchanganyiko wa antiseptiki kama vile savlon (chlorhexidene 2 -4%.] Ikiwa hauna kiowevu cha antiseptiki, tayarisha maji vuguvugu na sabuni.

Usitumie kileo kupanguzia uke!

Mwanamke aliyekuja kwenye Kituo cha Afya anaweza kuwa tayari katika awamu ya pili ya leba. Ikiwa hivyo, mpeleke kochini mara moja kisha umtulize. Ikiwa utamhudumia nyumbani, chagua mahali safi na salama. Tayarisha mapema vifaa unavyohitaji kutumia unapozalisha. Vipange na uviweke tayari.

Vifaa unavyohitaji wakati wa kuzalisha vimeelezwa katika Kipindi cha 3.

Chunguza dalili kuu

  • Shinikizo la damu: vipimo vya kawaida ni kati ya vipimo 90/60 hadi chini ya 140/90.
  • Kiwango cha mpwito wa ateri za mama: kiwango cha kawaida ni midundo 80-100 kwa dakika kwa mwanamke aliye katika leba. Kiwango kilicho juu ni midundo 110 kwa dakika.
  • Kiwangojoto cha mwili: wastani wa nyusi 37. Ikiwa kipo kati ya nyusi 37.5 - 38.4, mwanamke huyo ana homa ndogo. Ikiwa ni nyusi 38.5 au zaidi, ana homa kuu.

Ulijifunza jinsi ya kuanzisha kutoa viowevu vya vena katika Kipindi cha 22 kwenye moduli ya Utunzaji wa Kabla ya Kuzaa na Somo la ujuzi wa kiutendaji.

Iwapo mojawapo ya dalili hizi muhimu au dalili zote hizi zimepita hali ya kawaida, mpatie rufaa kwa dharura hadi kituo cha afya (Mchoro 2.1). Iwapo hali imezidi ile ya kawaida kwa kiwango kikubwa, anza kumwongeza viowevu mwilini. Unafaa kufanya hivi iwapo tu umepewa Somo la kufanya hivyo. Baadaye, mpatie rufaa hadi kwenye kituo cha afya.

Mchoro 2.1 Mpe rufaa kwa haraka mwanamke mwenye ishara muhimu zisizo za kawaida.

Mtazame na umsikize mwanamke huyu

  • Je, alibebwa alipokuwa akiletwa katika kituo cha afya?
  • Kuna damu kwenye nguo yake au sakafuni chini yake?
  • Je, anakoroma, kupiga kite ama kuinamisha kichwa?
Mchoro 2.2 Ikiwa mama anavuja damu kwa wingi, anahitaji usaidizi wa dharura.

Muulize yeye, au mtu aliye naye, kama amewahi kupata dalili zifuatazo, au kama anazo kwa sasa:

  • Kuvuja damu kutoka ukeni
  • Maumivu makali ya kichwa au kuona uluwiluwi
  • Mitukutiko ya mwili au kukosa fahamu
  • Matatizo ya kupumua
  • Homa
  • Maumivu makali ya fumbatio
  • Kuvuja kwa kiowevu cha amnioni kabla ya wakati (maji kuvunjika kabla ya wakati).

Ikiwa kwa sasa mwanamke ana mojawapo ya dalili hizi, chukua hatua zifuatazo mara moja:

  • Paza sauti kuomba usaidizi.
  • Tulia na uweke makini yako kwa mwanamke huyo.
  • Kaa naye wala usimwache pekee.
  • Mpe kwa haraka huduma zinazohitajika kabla ya rufaa kisha umfanyie rufaa hadi kwenye kituo cha afya kilicho karibu.

Utajifunza jinsi ya kushughulikia leba tata katika vikao vya 8-11 kwenye moduli hii. Utajifunza utaratibu wa kutoa rufaa na unachofaa kufanya ukiwa njiani kuelekea kituo cha afya.

2.1 Mchunguze kwa haraka mwanamke aliye katika leba

2.2 Chukua historia ya mwanamke aliye katika leba