2.2.1 Umuhimu wa huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke

Kanuni zinazozingatia maslahi ya mwanamke zimeonyeshwa katika Jedwali 2.1

Kisanduku 2.1 Huduma inayozingatia maslahi ya mwanamke aliye katika leba na kuzaa

  1. Kuwezesha kutolea huduma iliyo bora kwa mwanamke na ina viashirio vifuatavyo:
    • Huzingatia imani, tamaduni na desturi zake
    • Hutilia maanani hali ya mwanamke huyu ya kihisia, kisaikolojia na kijamii.
    • Huwezesha ushauri mwafaka.
  2. Kumhimiza mwanamke, na yeyote ambaye angependa kuwa naye wakati wa leba. Wote huhusika katika utunzaji wake. Jukumu lako ni kuwafunza jinsi ya kumtunza na kuwaelimisha wote kuhusu yale yote yanayoendelea.
  3. Kutilia maanani na kuheshimu haki za mwanamke:
    • Haki yake ya kuarifiwa kuhusu afya yake na ya mtoto.
    • Haki yake ya kuarifiwa kuhusu utaratibu wa leba na kuzaa na anachotarajia leba inapoendelea.
    • Haki yake ya kukubali au kukataa kufanyiwa uchunguzi na huduma zingine.
  4. Kuwahimiza wahudumu wote wa afya kutumia ustadi wa uhusiano mwema na kuwasiliana kikamilifu kwa lugha ambayo mwanamke anaweza kuelewa.

2.2 Chukua historia ya mwanamke aliye katika leba

2.2.2 Nakili data kuhusu demografia ya jamii.