2.2.4 Dalili na ishara hatari

Muulize mteja iwapo kuna dalili zozote hatari alizogundua. (Dalili ni hisia ambazo mtu hupata na anaweza kuzieleza. Ishara ni kitu ambacho mhudumu aliyehitimu pekee hutambua baada ya kufanya uchunguzi.)

  • Je, unaweza kukumbuka dalili hatari za ujauzito ulizojifunza katika Kipindi cha 17 cha moduli ya Utunzaji katika Ujauzito?

  • Dalili hatari ni pamoja na kuvuja damu ukeni, (nzito kuzidi damu tetelezi), maumivu ya kichwa mfululizo, kupoteza fahamu, maumivu makali katika epijastriamu na fumbatio. Dalili zingine hatari ni pamoja na kuvuja kwa kiowevu cha amnioni kabla ya leba na utetelezi usio wa kawaida kutoka kwenye uke. Ikiwa mwanamke atalalamika kuwa na mojawapo ya dalili hizi, mpatie rufaa kwa dharura hadi kituoni cha afya kilicho karibu.

    Mwisho wa jibu

2.2.3 Historia ya ujauzito uliopo na uliopita

2.3 Uchunguzi wa mwili wakati wa leba