2.3.1 Kuchunguza fumbatio

Ukichunguza fumbatio la mwanamke, tathmini ukubwa na umbo lake na kovu.

  • Ukubwa: Je, fumbatio lake ni kubwa sana au dogo sana ukilinganisha na umri wa fetasi? Ikiwa fumbatio lake ni dogo sana, inawezekana kuwa mtoto hajakua ipasavyo. Ikiwa ni kubwa sana, mwanamke anaweza kuwa na mapacha au hali inayoitwa polihidramniosi (uwepo wa kiowevu kingi cha amnioni). Ikiwa fumbatio ni kubwa au dogo sana, mpatie rufaa mwanamke hadi kwenye kituo cha afya.
  • Umbo: Je fumbatio lake lina umbo la yai, yaani pana kidogo katika sehemu ya juu ya uterasi na lembamba kwenye sehemu ya chini? Kuelekea kileleni mwa ujauzito, umbo hili huonyesha kwamba mtoto anatanguliza kichwa. Ikiwa fumbatio lina umbo la duara kama mpira, inaweza kuwa ishara kuwa mtoto yuko katika hali mbaya ndani ya uterasi. (Utajifunza kuhusu haya hapa na katika Kipindi cha 8)
  • Kovu: Je, mwanamke yuko na kovu katika sehemu ya chini ya uterasi kutokana na upasuaji wa awali (Mchoro 2.3)? Kwa kawaida, kovu hili huwa juu ya mfupa wa kinena. Uterasi inaweza kupasuka wakati wa kuzaa ikiwa ina kovu. (Utajifunza haya katika Kipindi cha 10).
Mchoro 2.3 Upasuaji wa awali unaongeza hatari katika leba ijayo.

2.3 Uchunguzi wa mwili wakati wa leba

2.3.2 Kuchunguza kwa kupapasa fumbatio