2.3.4 Kukadiria mikazo

Ili kukadiri marudio na muda wa mikazo, weka mkono wako juu ya fumbatio la mama, ukiuzungusha juu ya fandasi. Utahisi fumbatio likikazana na kuwa gumu. Mama anaweza kupiga kite wakati wa mkazo. Hesabu idadi ya marudio (idadi ya mikazo katika kila dakika 10) na muda (wakati baina ya mikazo ikihesabiwa kwa sekunde). Andika vipimo hivi katika chati inayoitwa patografu. Pia utanakili dalili muhimu za mama na vipimo vya kima mdundo wa moyo wa fetasi. (Ulijifunza kuhusu patografu katika Kipindi cha 4.)

2.3.3 Kupima kima cha mdundo moyo

2.3.5 Kuchunguza uke