2.3.6 Kuchunguza sehemu ya nje ya uzazi na uke

Ukadiriaji wa mwisho katika Kipindi hiki ni kuchunguza sehemu ya nje ya uzazi wa mama na pembeni mwa sehemu ya ndani ya uke ili kutambua dalili za hatari.

Katika moduli ya Huduma za baada ya Kuzaa, unajifunza jinsi ya kuweka dawa ya (tetracycline) macho ya mtoto mchanga ili kumkinga kutokana na uwezekano wa maambukizi na viini kutoka kwenye njia ya uzazi.

  • Kuna mchozo wowote usio wa kawaida (mzito, wenye rangi ya manjano au nyeupe, na wenye uvundo) kutoka ukeni. Kuna vidonda vilivyovimba kwenye sehemu ya nje ya uzazi? Dalili hizi zinaweza kusababishwa na maambukizi ya njia ya mkojo au ya zinaa.
  • Kuna kovu ukeni zinazotokana na majeraha aliyopata alipokuwa akizaa mara ya kwanza au kutokana na ukeketaji (tohara)? Kovu hizi huchangia kuongeza kwa hatari ya kupata fistula. (Fistula ni uwazi ulioraruka baina ya uke na viungo vingine)
  • Je, uke umevimba? Uke unaweza kufunga njia anayopitia mtoto?

Ukiona mojawapo ya hizi dalili hatari, mpe mwanamke huyo rufaa hadi kwenye kituo cha afya, isipokuwa wakati mtoto yuko karibu kuzaliwa. Kipindi cha somo kifuatacho kinaelezea jinsi ya kutunza mwanamke aliye katika leba.

2.3.5 Kuchunguza uke

Muhtasari wa Kipindi cha 2 cha Somo