Muhtasari wa Kipindi cha 2 cha Somo

Katika Kipindi hiki, umejifunza:

  1. Kutayarisha vifaa vyako mapema kushughulikia leba na kuzaa, ili uwe tayari kuondoka punde tu unapoitwa.
  2. Kuchunguza upesi ishara muhimu (shinikizo la damu, kiwango cha mpito wa ateri na kiwangojoto cha mwili) za mwanamke katika leba.
  3. Kufuata kanuni za utunzaji usimwathiri mwanamke. Heshimu imani, matakwa na haki zake. Mhimize yeye na wanaomtunza nyumbani wamhudumie wakati wa leba na kuzaa.
  4. Kuuliza habari kuhusu mwanamke huyo na kuinakili: jina, umri, anwani, ugravida na usawa, siku ya mwisho kuona hedhi, mara ya kwanza kuhisi fetasi ikisonga, na muda uliopita baada tangu mkazo wa kwanza.
  5. Kuuliza kuhusu dalili za hatari: kuvuja damu ukeni, maumivu ya kichwa, mtukutiko wa maungo, matatizo ya kupumua, homa, maumivu makali ya fumbatio, kuvuja kwa kioevu cha amnioni kabla ya wakati wake (kupasuka kwa maji).
  6. Kutumia zile maneva nne za Leopold katika kupapasa fumbatio. Kutambua kutanguliza na hali fetasi, na jinsi ambavyo sehemu inayotanguliza ilivyofungamana.
  7. Kuchunguza uke wa mwanamke aliye katika leba. Kadiria kiwango cha kupanuka kwa seviksi, jinsi fetasi ilivyotanguliza, na kiwango ambacho fetasi imeshuka. Kadiria fuvu la fetasi, na utafute dalili za maambukizi ya uke, kovu au uvimbe.

2.3.6 Kuchunguza sehemu ya nje ya uzazi na uke

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 2 cha Somo