Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 2 cha Somo

Kwa vile umekamilisha Kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili kuthibitisha jinsi ulivyotimiza Malengo ya Somo la Kipindi hiki. Andika majibu yako katika shajara yako ya somo kisha uyajadili na mkufunzi wako katika mkutano wa Kipindi kifuatacho. Linganisha majibu yako na Maandishi ya Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni mwa moduli hii.

MK 2.1 (linatathmini Malengo ya Mafundisho)

Chukulia kwamba umeitwa nyumbani mwa mwanamke wa umri wa chini aliye katika leba. Ni nini unachofaa kufanya kwa dharura?

Answer

Mtathmini mwanamke huyo upesi ili kuamua kama ni lazima kumpa rufaa ya huduma kwa dharura.

  • Chunguza mdundo wa moyo wa fetasi. (Je, vipo katika hali ya kawaida ya midundo 120-160 /dakika?)
  • Chunguza dalili muhimu (shinikizo la damu, kiwango cha mpwito wa ateri na kiwango joto) ili kuona kama zipo katika hali ya kawaida. (Kifungu cha 2.1.1).
  • Tafuta dalili za kuvuja damu au kioevu cha amnioni.
  • Muulize (au aliye naye) ana maumivu ya kichwa au kuona uluwiluwi, matatizo ya kupumua, mtukutiko wa maungo, au maumivu makali ya fumbatio.

Ukiona dalili za dhikisho la fetasi, ikiwa moja wapo ya ishara muhimu zipo katika hali isiyo ya kawaida, au kukiwepo na mojawapo ya dalili hatari, mpe rufaa kwa hapo. (Dalili ya matatizo ya fetasi ni mdundo wa moyo ulio katika hali isiyo ya kawaida.)

Mwisho wa jibu

MK 2.2 (linatathmini Malengo ya Somo)

Umepapasa fumbatio la mwanamke aliye katika leba. Jaza mapengo yaliyo katika Kisanduku 2.1.

Kisanduku 2.1 Maneva za Leopold

Jina la papasoSehemu ya fumbatio inayopapaswaUnachofaa kuchunguza
Papaso la fandasi

Mikono ikiwa imewekwa kwenye pande zote za sehemu ya kati ya fumbatio, mkono mmoja ukifuatwa na mwingine ikisumia ndani

Ukitazama upande wa miguu, mikono ikiwa upande wa chini ya fumbatio, sukuma juu tu ya mfupa wa kinena, ukielekeza ndani kwa vidole vyako

Iwapo kichwa cha fetasi kimefungamana kwenye seviksi. Ukiweza kushika kichwa kutumia upana wa vidole viwili juu ya mfupa wa kinena cha mama, kichwa kimefungamana.

Answer

Kisanduku 2.1 maneva ya Leopold Imekamilika

Jina la papasoSehemu ya fumbatio itakayo papaswaCha kuangalia
Papaso la fandasiMikono ikiwa karibu na sehemu ya juu ya fumbatio ya mama, sukuma vidole vyako ukizungushia fandasi ya uterasiHali ya fetasi – Ikiwa iko katika hali ya longitudo (kawaida), mshazari au kukingama
Papaso la pembeniMikono ikiwekwa bapa kwenye sehemu zote mbili za katikati ya fumbatio; mkono wa kwanza ukifuatwa na wa pili kusukuma ndani.Uaguaji kamili wa mtoto alivyo lala na kama ni ‘kichwa chini’ au kutanguliza tako
Papaso la ndani zaidi la pelvisiTazama kuelekea miguu ya mama, mikono ikiwa upande wa chini ya fumbatio lake, sukuma ndani kwa vidole juu ya mfupa wa kinena kidogo. Ili kuhakikisha hali ya kichwa (kichwa chini) kutanguliza kichwa au (chini kabisa) kitangulizi
Mshiko wa PawlickVidole vinashikilia kichwa cha fetasi juu ya mfupa wa kinena kidogo.Kama kichwa cha fetasi kimefungamana na seviksi. Ikiwa Unaweza kushika kichwa kwa upana wa vidole juu ya mfupa wa kinena wa mama, kichwa kimefungamana.

Mwisho wa jibu

MK 2.3 (linatathmini Malengo ya Somo)

Makeda ametembelea Kituo chako cha Afya. Umemchunguza upesi kisha ukabaini kuwa hatahitaji rufaa ya dharura. Sasa unachukua historia yake. Utachukua vipi historia yake na ni habari gani unayofaa kupata kutoka kwake?

Answer

(a) Ili kuchukua historia ya Makeda, mhimize kuwa na uwazi wa kuzungumza nawe. Fuata kanuni za utunzaji mwafaka kwa mwanamke unapomuuliza maswali. Sikiza kwa makini, jibu maswali yake na uweke siri anayokufichulia. (Tazama Ksanduku 2.1 ili kupata maelezo kuhusu huduma mwafaka kwa mwanamke.)

(b) Ujumbe unaohitaji kutoka kwa Makeda:

  • Jina lake, umri, kimo, anwani, dini (iwapo anataka kukwambia) na kazi (iwapo ameajiriwa).
  • ‘Dalili yake tangulizi’ ni nini (kwa mfano leba, kuhisi uchovu)?
  • Je, ameshawahi kupata mimba au kuzaa tena? (Alikuwa na matatizo yoyote? Ni matatizo mangapi iwapo alikumbana nayo?)
  • Siku ya kwanza ya kipindi kilichopita cha hedhi ya kawaida ilikuwa gani?
  • Je, ametambua dalili zozote hatari (kwa mfano kuvuja damu kutoka ukeni, maumivu ya kichwa, mchozo usio wa kawaida kutoka ukeni)?

Mwisho wa jibu

MK 2.4 (linatathmini Malengo ya Somo 2.6 na 2.7)

Sasa umepata historia ya Makeda na unataka kumchunguza. Je, utafanya nini kwanza na ni nini unachochunguza?

Answer

Kabla ya kumchunguza ukeni, fuata kanuni za utunzaji mwafaka wa mwanamke na umwakikishie Makeda kuhusu siri zake. Kisha nawa mikono kabisa na uvae glavu mpya. Chunguza yafuatayo wakati unapochunguza:

  • Kiasi ambacho seviksi imepanuka.
  • Kiasi cha pelvisi ya Makeda na iwapo fetasi itaweza kupita
  • Kiwango cha kufinyangika (kupishana) kwa mifupa ya fuvu la fetasi kufuatia shinikizo kwenye njia ya uzazi.
  • Mchozo wowote unaonuka na usio wa kawaida; kovu yoyote au kufura. (Dalili hizi ni hatari. Ukizitambua dalili hizi, mhamishe Makeda hadi kwenye kituo cha afya.)

Mwisho wa jibu

MK 2.5 (linatathmini Malengo ya Somo la 2.1)

Ni maelezo gani yasiyo ya kweli? Katika kila kauli, eleza lisilo la kweli.

  1. Kiwangojoto cha mwili cha nyusi 39 ni dalili ya homa ya kiwango cha juu.
  2. Umri wa ujauzito ni miaka aliyo nayo mama wakati anapokuwa mjamzito.
  3. Usawa ni idadi ya watoto waliozaliwa hai baada ya wiki 28 za ujauzito.
  4. Ugravida ni idadi ya mimba amewahi kupata bila kuzingatia Malengo ya mimba hiyo.
  5. Unapochunguza fumbatio la mwanamke aliye katika leba, angalia ukubwa, umbo na kovu.
  6. Kuchunguza kwa kupapasa fandasi mlio kama wa ngoma unaosikia unaposikiza moyo wa mtoto ukitumia fetoskopu.
  7. Kutanguliza matako ni ishara kuwa utaratibu wa kuzaa utakuwa na matatizo.
  8. Oskulesheni ni milio ambayo mama aliye katika leba kwa wakati mwingine hutoa.

Answer

  1. A ni kweli. Homa ya kiwango cha juu ni kiwangojoto kilichozidi nyusi 38.5 (homa ya kiwango cha chini ni kati ya nyusi 37.5 - 38.4.)
  2. B si kweli. Umri wa ujauzito ni idadi ya wiki ambazo fetasi imekuwa ndani ya uterasi. Muda huu huhesabiwa kutoka siku ambayo kipindi cha mwisho cha hedhi ya kawaida kilianza.
  3. C si kweli. Usawa ni idadi ya watoto waliozaliwa baada ya wiki 28 za ujauzito.
  4. D si kweli. Ugravida ni idadi ya mimba amewahi kupata bila kuzingatia Malengo ya mimba hiyo.
  5. E ni kweli. Kovu isiyo ya kawaida ni ishara kuwa uterasi inaweza kuwa na kovu, jambo linaloongeza hatari ya kupasuka kwa uterasi.
  6. F si kweli. Kuchunguza kwa kupapasa fandasi ni jina lililopewa utaratibu wa kupapasa sehemu ya chini ya uterasi yenye umbo la kuba (inayojulikana kama fandasi) ili kutambua hali ya kichwa cha mtoto.
  7. G si kweli. Kutanguliza matako ni wakati matako ya mtoto ndiyo sehemu iliyotangulia. Kutanguliza matako ni ishara kuwa utaratibu wa kuzaa unaweza kuwa na matatizo. Unafaa kumhamisha mwanamke huyu hadi kwenye kituo cha afya.
  8. H si kweli. Oskulesheni ni kusikiza sauti zilizo ndani ya fumbatio.

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 2 cha Somo