Malengo ya Somo la Kipindi cha 3

Baada ya kuhitimisha somo hili, unatarajiwa:

3.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandikwa kwa herufi nzito. (Swali la Kujitathmini 3.7)

3.2 Kukadiria mahitaji ya mwanamke aliye katika leba na kumtunza ifaavyo. (Maswali ya Kujitathmini 3.1 na 3.7)

3.3 Kumpa mwanamke aliye katika leba usaidizi wa kihisia na kisaikolojia. (Swali la Kujitathmini 3.1)

3.4 Kufuatilia hali ya mama na fetasi katika awamu ya kwanza na ya pili ya leba na kurekodi habari hiyo. (Maswali ya Kujitathmini 3.2, 3.3, 3.5 na 3.6)

3.5 Kutayarisha vifaa vya uzalishaji wa kawaida. (Swali la Kujitathmini 3.4)

3.6 Kutwaa hadhari za kiwango cha usafi kinachohitajika na kinga dhidi ya maambukizi katika utunzaji wa kuzalisha. (Swali la Kujitathmini 3.4 na 3.7)

Kipindi cha 3 Kumtunza Mama aliye katika Leba

3.1 Kukadiria mahitaji ya mwanamke aliye katika leba