3.1 Kukadiria mahitaji ya mwanamke aliye katika leba

Kila mwanamke huhitaji usaidizi wa aina tofauti. Hata hivyo wanawake wote huhitaji wema, heshima na usikivu. Mtazame na umsikilize ili ufahamu hisia zake. Mhimize ili ahisi kuwa mwenye nguvu na ujasiri wakati wa leba. Msaidie kutulia na kuanza kuipokea leba yake.

Mchoro 3.1 Msaidie mwanamke aliye katika leba kutulia.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 3

3.1.1 Kuifadhili leba