3.1.2 Kuikinga leba

Kukinga leba ni kuilinda dhidi ya madhara.

Hakikisha kuwa watu wote fidhuli na wasio wakarimu hawamsumbui mama. Mama huyu hapaswi kuhofishwa na shida za kifamilia. Wakati mwingine hata marafiki wa kufadhili na kuonyesha upendo wanaweza kudhuru leba. Wakati mwingine, mbinu mwafaka katika kuzalisha ni kuwaeleza watu wote waondoke chumbani ili mama asiwe na wasiwasi wakati wa leba.

Usitumie dawa au taratibu zisizohitajika! Usimpe mama dawa za kuharakisha leba kwa kuwa dawa hizi huongeza hatari.

Watu wengine huamini kwamba dawa, vifaa na uchunguzi zaidi kwa mama humfanya azae kwa njia salama zaidi. Kwa kawaida fikira hii si kweli. Hatua hizi zinaweza kufanya uzalishaji kuwa mgumu au kusababisha matatizo. Sindano au tembe zinazopewa akina mama ili kuharakisha kuzaa zinaweza kufanya leba kuwa chungu zaidi na hata kusababisha kifo cha mama na mtoto.

3.1.1 Kuifadhili leba

3.1.3 Mkao na mwendo