3.1.4 Kumsaidia mama kudhibiti mikazo yake

Huenda mama aweze kupata usingizi katika vipindi vya kwanza vya leba. Wanawake wengi huhisi uchovu mikazo yao ikiwa dhabiti sana. Wao wanaweza kuhofia kuwa hawana nguvu za kutosha kumsukuma mtoto. Hata hivyo uchovu wa mwili ni hali ya mwili kumpuzisha na kumtuliza mama. Iwapo mambo yote ni salama, mama atakuwa na nguvu za kuzaa wakati utakapofika.

Ili kuhifadhi nguvu zake, mama anapaswa kutulia katikati ya mikazo na hata punde leba inapoanza. Hii inamaanisha kuwa mikazo inapokoma, mama anapaswa kuuacha mwili wake kupumzika, avute pumzi nyingi na wakati mwingine aketi au kulala.