3.1.8 Kutumia vinywaji wakati wa leba

Mwanamke aliye katika leba hutumia nguvu nyingi na maji ya mwili kwa haraka. Katika awamu ya kwanza ya leba, mwanamke anapaswa kunywa angalau kikombe kimoja cha kinywaji kilicho na kiwango cha juu cha kalori kila saa, kama vile chai, vinywaji visivyolevya, supu au maji ya matunda. Mwanamke huyu asipokunywa vinywaji vya kutosha, anaweza kuishiwa na maji (kukosa maji ya kutosha mwilini). Jambo hili linaweza kufanya leba kuwa ndefu na ngumu zaidi na kumfanya kuhisi uchovu. Ukosefu wa maji mwilini pia unaweza kumfanya mwanamke huyu kujihisi mchovu.

Dalili za kuishiwa na maji ni pamoja na:

  • Midomo iliyokauka
  • Macho yaliyobonyea
  • Ngozi kupoteza unyoofu.
  • Homa ndogo (hadi nyusi 38)
  • Pumzi nzito na za haraka (pumzi za zaidi ya mara 20 kila dakika)
  • Mpwito dhaifu wa moyo, lakini wa haraka (zaidi ya midundo 100 kila dakika)
  • Mpigo wa moyo wa mtoto ni haraka kuliko midundo 160 kila dakika.

3.1.7 Kupumua wakati wa leba

3.1.9 Kutunza kibofu