3.1.9 Kutunza kibofu

Mshawishi mama mjamzito kukojoa angalau mara moja kila baada ya saa 2 (Mchoro 3.5a). Mikazo huwa dhaifu na leba kuchukua muda mrefu zaidi, iwapo kibofu kimejaa. Kibofu kilichojaa kinaweza pia kusababisha maumivu, matatizo wakati wa kusukuma plasenta na kuvuja damu baada ya kuzaa. Mkumbushe mama kukojoa, kwa sababu anaweza kusahau.

Mchoro 3.5 (a) Mshawishi mama kukojoa angalau kila baada ya saa 2. (b) Kibofu kilichojaa kinaweza kusababisha maumivu na kufanya leba kuchukua muda mrefu zaidi.

Gusa sehemu ya chini ya tumbo ya mama ili kuchunguza kama kibofu kimejaa. Kibofu kilichojaa huwa kama mfuko wa plastiki uliojaa maji. Unaweza kuona umbo la kibofu chini ya ngozi ya mama ikiwa kimejaa sana (Mchoro 3.5b). Usingoje hadi kibofu chake kijae sana.

Ni lazima mama akojoe iwapo kibofu chake kimejaa. Ikiwa hawezi kutembea, jaribu kumwekea sinia au pedi chini yake na umwagize akojoe. Ili kumsaidia kuanza kukojoa, weka mikono yake ndani ya maji vuguvugu.

  • Unafikiri ni kwa nini kibofu kilichojaa kinaweza kutatiza hali ya kawaida ya leba? (Fikiri kuhusu yale unayojua kutoka katika vipindi viwili vya somo vilivyopita.

  • Katika awamu ya kwanza na ya pili ya leba, kibofu kilichojaa kinaweza kutatiza mikazo ya kawaida ya uterasi. Kibofu kilichojaa huweka kichwa cha mtoto nje ya ukingo wa uterasi.

    Mwisho wa jibu

Katika Kipindi cha 6, unajifunza kuwa katika awamu ya tatu ya leba kibofu kilichojaa kinaweza kuchelewesha kutolewa kwa plasenta. Kuchelewa huku huongeza hatari ya kuvuja damu baada ya kuzaa (Kipindi cha 11).

3.1.8 Kutumia vinywaji wakati wa leba

3.1.10 Usaidizi wa kihisia na kisaikolojia kwa mwanamke aliye katika leba