3.2.1 Tathmini jinsi leba inavyoendelea

Leba huwa tofauti. Zipo leba za kasi na zingine taratibu. Jambo hili ni la kawaida. Lakini leba salama inafaa kuendelea. Kuendelea kunamaanisha kuwa leba inaendelea kuwa thabiti zaidi na seviksi hufunguka. Kisanduku 3.1 linatoa kwa muhtasari sifa kuu za leba inayoendelea kwa kawaida.

Mchoro 3.6 Mhakikishie mama huyu kuwa mikazo inazidi kuwa thabiti zaidi kwa sababu leba ni ya kawaida.

Kisanduku 3.1 Kuendelea taratibu kwa leba ya kawaida

  • Mikazo huchukua muda zaidi, kuwa thabiti zaidi na kufuatana kwa karibu zaidi.
  • Wakati wa mkazo, uterasi huwa ngumu zaidi ukiigusa (Mchoro 3.6).
  • Kiasi cha “utetelezi” huongezeka.
  • Mfuko wa maji hupasuka
  • Mama huteuka, kutoa jasho na kutapika, au miguu yake hutetemeka.
  • Mama huhisi haja ya kusukuma chini kupitia sehemu ya chini ya fumbatio

Katika Kipindi cha 4 cha Somo, unajifunza jinsi ya kutumia chati inayoitwa patografu. Chati hii hutumika kutathmini jinsi leba inavyoendelea na kunakili uchunguzi na vipimo vyako kwa usahihi. Lakini kwanza fahamu yanayoendelea mwilini mwa mwanamke. Pia unajifunza mambo muhimu ya kuchunguza wakati wa leba.

3.2 Ufuatilizi wa mama na fetasi wakati wa leba

3.2.2 Mikazo ya Uterasi