3.2.5 Michozo kutoka ukeni

“Utetelezi” ni jina la damu iliyo na kamasi inayooenekana katika leba ya mapema. Mtiririko wa damu unaweza kutokea kufikia mwisho wa awamu ya kwanza. Kiowevu cha amnion kinaweza kutirika kutoka ukeni baada ya tando kuraruka. Kiowevu hiki kinaweza kuwa na mekoniamu. Huu ni mchozo wa rangi ya kijani kibichi, ambao ni kinyesi cha kwanza cha mtoto. Ikiwa kiowevu cha amnioni kina mekoniamu, basi fetasi inaweza kuwa katika hali ya kufadhaika. Kwa kawaida, mtoto mchanga hutoa kinyesi baada ya kuzaliwa. Baadaye katika Moduli hii, utajifunza hatua za kuchukua ikiwa fetasi au mama yuko katika hali ya kufadhaika.

3.2.4 Kushuka kwa sehemu tangulizi

3.2.6 Hali ya Fetasi