3.2.7 Hali ya mama

Hesabu mipigo ya moyo wa mama baada ya kila dakika 30 na upime shiniko la damu na halijoto kila baada ya saa 4. Ulijifunza jinsi ya kuchukua vipim hivi katika Kipindi cha 9 cha Somo cha Moduli ya Utunzaji wa Wakati wa Ujauzito. Pia, nakili kwenye chati yako hesabu ya kula, kunywa na kukojoa.

Shinikizo la damu kushuka

Mwanamke huyu anapaswa kwenda hospitalini mara moja ikiwa shinikizo la damu litashuka ghafla!

Ikiwa shinikizo la damu la diastoli (nambari ya chini) litashuka ghafla kwa alama 15 au zaidi, mabadiliko haya ni athari ya hatari. Mabadiliko haya humaanisha kuwa mama anavuja damu sana. Ikiwa havuji damu kutoka ukeni, basi plasenta yake inaweza kuwa imetengeka na huenda akawa anavuja damu ndani ya uterasi (kuvuja damu wakati wa kuzaa).

Shinikizo la damu kupanda

Shinikizo la damu la mmHg 140/90 au zaidi ni ishara ya hatari. Mwanamke anaweza kuwa na priekilampsia. Priekilampsia inaweza kusababisha mitukutiko (eklampsia), kutengeka kwa plasenta, kuvuja damu ubongoni, au kuvuja damu nyingi sana. Mama na mtoto wanaweza kufa. Katika Kipindi cha 19 cha Somo cha Moduli ya Utunzaji wa Wakati wa Ujauzito sehemu ya 2, ulijifunza kuhusu eklampsia na priekilampsia. Nakili shinikizo la damu na vipimo hivi vingine katika patografu. Utajifunza jinsi ya kufanya hivyo katika kipindi kijacho.

Sasa utajifunza kuhusu vifaa unavyopaswa kutayarisha ili utumie kuzalisha.

3.2.6 Hali ya Fetasi

3.3 Jitayarishe kuzalisha