3.3.2 Tayarisha mahali pa kuzalishia
Ukishadhibitisha kuwa mwanamke yuko katika awamu ya pili ya leba, fanya maandalizi ya kwanza ya kuzalisha. Chumba cha kuzalishia kinafaa kuwa na kiwango mwafaka cha joto na mwangaza ili kuhakikisha kuwa msamba na vulva inaonekana vyema. Fuata utaratibu wa kuzuia maambukizi kama ilivyoelezwa katika Sehemu ya 3.5 ili kuandaa mahali safi pa kumpokea mtoto (Mchoro 3.7). Tandika vazi linalozuia maji kitandani na sakafuni . Hakikisha kuwa nguo za kumpasha mtoto joto zimetayarishwa.
3.3.1 Ishara za awamu ya pili ya leba