3.3.3 Vifaa na nyenzo unazohitaji ili kuzalishia

Hakikisha kuwa una nyenzo na vifaa unavyohitaji ili kuzalisha (Kisanduku 3.2 na Mchoro 3.8) katika Kituo cha Afya. Iwapo utamzalisha mwanamke nyumbani, nenda na vifaa hivyo. Ingawa mwanamke anaweza kuwa na vifaa vidogo vidogo, kama vile sabuni na vitambaa safi, unafaa kuwa umejiandaa vya kutosha. Tumia Kisanduku 3.2 kama orodha ya kukagulia. Hakikisha kuwa vifaa vyote viko unapapakia.

Kisanduku 3.2 Orodha ya kukagua vifaa vya kuzalisha

  • Maji safi, sabuni na taulo ya mkononi.
  • Aproni, miwani, kinyago na gauni.
  • Glavu safu.
  • Uzi safi mpya wa kufungia kitovu.
  • Wembe mpya au makasi yaliyotakaswa.
  • Fosepsi mbili aina ya klempu za kushikilia kambakitovu kabla ya kuikata.
  • Kitega kamasi au balbu ya kufyonzea kamasi kutoka kwenye matundu ya pua la mtoto (iwapo itahitajika).
  • Shashi iliyotakaswa, kijitambaa cha pamba na pedi ya kiafya ya mama kutumia.
  • Taulo mbili za mtoto zilizosafi na kavu, na vitambaa viwili vya kufunikia.
  • Stethoskopu na sijafu ya kupimia shinikizo la damu.
  • Kiowevu cha antiseptiki ili kusafishia msamba na viungo vya uzazi.
  • Vipimo 10 vya dawa ya kudungwa aina ya oxytocin ama mikrogramu 600 za tembe za misoprostol. Dawa hizi hutumika kuzuia damu kuvuja baada ya kuzaa. Oxytocin ndiyo dawa inayopendekezwa zaidi ingawa misoprostol inaweza kutumika ikikosekana. (Utajifunza zaidi kuhusu dawa katika Kipindi cha 6 cha Somo.)
  • Lihamu ya macho aina ya Tetracycline. (Antibiotiki hii ya macho hutumika kumkinga mtoto mzawa dhidi ya maambukizi ya macho.)
  • Ndoo tatu au vijibakuli vitatu vilivyo na kiowevu cha klorini au cha sabuni na maji safi katika kila kimoja. (Unaweza kutumia Berekina kutayarisha 0.5% ya kiowevu cha klorini. Soma ukolezi wake kwenye chupa. Iwapo ukolezi ni 5%, unaweza kutayarisha kiowevu chenye ukolezi wa 0.5% kwa kuchanganya kikombe 1 cha Berekina na vikombe 9 vya maji safi.)
  • Bakuli ya plastiki ya kumpokea mtoto.
Mchoro 3.9 Vifaa unavyohitaji ili kuzalisha.

3.3.2 Tayarisha mahali pa kuzalishia

3.4 Kuzuia maambukizi unapozalisha