3.4 Kuzuia maambukizi unapozalisha

Maambukizi husababisha magonjwa na hata kuua. Maambukizi ni baadhi ya visababishi vya vifo baada vingi baada ya kuzaa. Hatua nyingi unazochukua wakati wa leba na kuzalisha zinaweza kuwa salama iwapo tu utafuata kanuni za kimsingi za kuzuia maambukizi. Kanuni hizi zinaweza kuorodheshwa kwa muhtasari kama ”safi tatu”: mikono safi, mahali safi (pa kuzalisha) na vifaa safi. Tayari unafahamu kuwa unafaa kusafisha kabisa mahali pa kuzalisha. Hali kadhalika, fuata kanuni zingine za usafi kama zilivyoelezwa katika sehemu ifuatayo.

3.3.3 Vifaa na nyenzo unazohitaji ili kuzalishia

3.4.1 Kunawa mikono