3.4.1 Kunawa mikono

  • Je, kunawa mikono huzuia maambukizi vipi?

  • Kunawa mikono ni mojawapo ya mambo muhimu zaidi unaweza kufanya ili kuzuia maambukizi. Kunawa mikono hukuzuia kueneza viini vya magonjwa kwa watu wengine na kukukinga dhidi ya viini wewe mwenyewe.

    Mwisho wa jibu

Iwapo kuna jambo unalohitaji kufanya ili kuzuia maambukizi, basi ni kunawa mikono (Mchoro 3.10 na Kisanduku 3.3).

Mchoro 3.10 Jinsi ya kunawa mikono kwa dakika 2.

Kisanduku 3.3 Nawa mikono kila wakati kwa dakika mbili

Kabla yaBaada ya
Kuguza uke wa mama.Kusafisha uke baada ya kuzalisha.
Kunchunguza uke au pelvisi.Kuguza damu au viowevu vyovyote vingine.
Kumtoa mtoto.Haja ndogo au Haja kubwa.
Kumchunguza mtoto.

Kinawa mikono cha gliserini na alkoholi

Iwapo huna maji ya kunawia mikono, unaweza kuandaa kinawa mikono rahisi kinachojulikana kama kisugua mikono. Kinawa mikono hiki huua viini vilivyo mikononi iwapo kitatumiwa vyema.

Changanya mililita 2 za gliserini na mililita 100 za ethili au kileo aina ya aisopropili (ukolezi ni 60% hadi 90%). Kama sivyo, unaweza kutumia alkoholi yoyote inayotumika kusafisha ngozi kabla ya kudunga sindano.

Sugua mililita 5 hivi (kijiko 1 kidogo) za kisugua mikono ili kuisafisha mikono. Sugua mikono kwa makini huku ukisafisha sehemu za katikati ya vidole na ndani ya kucha. Endelea kusugua hadi mikono ikauke. Usikamue mikono yako au kuipanguza kwa kitambaa.

Ili kuzuia kuongezeka kwa kinawa mikono kwenye mikono, nawa mikono kwa sabuni na maji baada ya kukitumia mara 5-10.

Usitumie kisugua mikono iwapo mikono yako imechafuliwa na viowevu vya mwili ama ina uchafu unaoonekana; badala yake, nawa mikono kwa sabuni na maji.

3.4 Kuzuia maambukizi unapozalisha

3.4.2 Vaa mavazi ya kujikinga