3.4.4 Mahali safi pa kuzalisha na utaratibu mwafaka wa kutupa uchafu

Sugua mahali pa kuzalisha hadi pawe safi. Hakikisha kuwa vitambaa vyote, taulo na vitambaa vya kufunikia ni safi na kavu. Shuka zote anazolalia mama na zile unazomfunikia mtoto wakati wa kumwosha zinafaa kuwa safi kabisa.

Baada ya kuzalisha, weka uchafu wote kwenye chombo kisichovuja kama vile mkebe wenye kifuniko imara. (Uchafu huu ni kama vile damu, shuka chafu, tando na plasenta.) Kitupe chombo hiki mahali salama ambapo hakiwezi kuonekana. Choma au uzike uchafu. Ni muhimu kuzuia maambukizi yaliyo kwenye uchafu huu kuenea kwenye jamii.

Jitahadhari na sindano. Weka sindano ndani ya kijisanduku salama baada ya kutumia sirinji inayotupwa. Usiwache sindano kutapakaa ovyo.

3.4.3 Safisha na uvitakase vifaa kwa kiwango cha juu

3.5 Hitimisho