3.5 Hitimisho

Ulijifunza jinsi ya kumsaidia mwanamke aliye katika leba, vifaa vinavyohitajika na jinsi ya kutupa uchafu. Katika kipindi kijacho, utajifunza kuhusu kuzaa kwenyewe na jinsi ya kutumia patografu.

Katika Kipindi cha 3, ulijifunza yafuatayo:

  1. Wanawake huhitaji utunzaji wa kibinafsi wakati wa leba na kuzaa. Wanawake wajawazito wanafaa kutafuta msaada kwa mhudumu aliyehitimu.
  2. Mpe mwanamke aliye katika leba pamoja na mtu aliyeambatana naye usaidizi wa kimwili, kihisia na kisaikolojia.
  3. Msaidie kutumia mikao tofauti, kujaribu njia tofauti za kupumua, kukubali kusuguliwa mgongo na kutoa sauti ndogo wakati wa leba. Hatua hizi hupunguza uchungu na kudhibiti mikazo.
  4. Mshauri kunywa angalau kikombe kimoja cha kiowevu kila siku. Msaidie kukojoa angalau mara moja kila baada ya masaa 2.
  5. Mjulishe jinsi leba inavyoendelea ili atulie na awe mjasiri.
  6. Fuatilia hali ya fetasi. Chunguza mpigo wa moyo wa fetasi kila baada ya dakika 30. Kiwango cha mpigo wa moyo kinafaa kuwa cha kawaida.
  7. Fuatilia hali ya mama. Pima kiwango chake cha shinikizo la damu na kiwango joto cha mwili kila baada ya masaa 4, na mpigo wa mishipa kila baada ya dakika 30.
  8. Chunguza jinsi leba inavyoendelea. Chunguza urefu, uthabiti na marudio ya mikazo ya uterasi kila baada ya dakika 30. Chunguza jinsi kichwa kinavyoshuka kila baada ya saa 2. Chunguza jinsi seviksi inavyopanuka kila baada ya saa 4.
  9. Tayarisha vifaa unavyohitaji kutumia kuzalisha. Jumuisha nguo za kujikinga mwenyewe. Sugua au utakase kila kitu kinachoguzana na tishu au viowevu vya mwili.
  10. Tumia sabuni na maji safi kunawa mikono. Nawa mikono ili kupunguza hatari ya kumwambukiza mama na mtoto wakati wa leba na kuzaa.

3.4.4 Mahali safi pa kuzalisha na utaratibu mwafaka wa kutupa uchafu

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 3