Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 3

Kwa kuwa sasa umekamilisha kipindi hiki, jibu maswali yafuatayo ili kubaini jinsi ulivyotimiza Malengo ya Somo ya kipindi hiki. Andika majibu yako kwenye Shajara yako ya Masomo na uyajadili na Mkufunzi wako katika Somo Saidizi kijacho. Unaweza kulinganisha majibu yako na uliyoandika kwenye Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.

Uchunguzi Maalum 3.1. Woizero Almaz

Woizero Almaz ni mwanamke aliye katika hatima ya kipindi cha ujauzito. Alikuja katika Kituo cha Afya akiwa na maumivu na kutokwa na mchozo ulio na damu ukeni mwake. Maumivu yalianza saa 5 zilizopita. Ana wasiwasi kuhusu mimba yake, kwa sababu ni yake ya kwanza. Unapomchunguza, unatambua kuwa yuko katika awamu yake ya kwanza.

Swali la Kujitathmini 3.1 (linatathmini Matokeo ya Somo la 3.2 na 3.3)

Ni usaidizi gani unaoweza kumpa Woizero Almaz ili kumtuliza kuhusu hali yake?

Answer

Ili kumhakikishia Almaz, kuwa mkarimu na uziheshimu mila na kaida zake ili akuamini. Onyesha kuhusika katika hali yake. Mweleze kinachoendelea kuhusu leba yake. Mhimize kuuliza maswali na kujieleza kuhusu mawazo na wasiwasi alionao. Mweleze kuhusu hali ya mtoto. Mruhusu msaidizi kukaa naye. Mweleze kuhusu kila hatua kabla ya kuitekeleza.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.2 (linatathmini Matokeo ya Somo la 3.4)

Ni vifaa gani vya kukadiria unavyotumia kuchunguza jinsi leba yake inavyoendelea? Vifaa hivi vinakusaidia aje?

Answer

Pima shinikizo la damu, halijoto na mpigo wa mishipa ya Almaz ili kufahamu kuhusu hali yake. Chunguza mpigo wa moyo wa fetasi kubaini ikiwa anafadhaika. Fuatilia mikazo, kupanuka kwa seviksi na kushuka kwa kichwa cha mtoto ili kutathmini jinsi leba inavyoendelea. (Ulijifunza kuhusu patografu katika Kipindi cha 4 cha Somo. Kifaa bora zaidi cha kufuatilia jinsi leba inavyoendelea na kubaini tatizo lolote kwa haraka ni patografu).

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.3 (linatathmini Matokeo ya Somo la 3.5 na 3.6)

Katika kipindi cha kwanza cha leba, ni aina gani ya chakula unachomshauri atumie? Ni mara ngapi unajaribu kumshawishi ale?

Answer

Katika awamu ya kwanza ya leba, mwanamke anashauriwa kula chakula kilicho na kiwango cha juu cha kalori. Baadhi ya mifano ni kama chai, vinywaji vyepesi, supu na maji ya matunda. Almaz anapaswa kunywa kikombe kimoja angalau baada ya kila saa 1.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.4 (linatathmini Matokeo ya Somo la 3.5 na 3.6)

Unapomhudumia Almaz wakati wa leba, unazuia vipi maambukizi?

Answer

Unapochunguza uke na kuzalisha, tumia hatua za kawaida za tahadhari na uzuiaji wa maambukizi. Kabla ya na baada ya kila hatua, nawa mikono angalau kwa dakika 2. Tumia sabuni na maji safi au kinawa mikono cha alkoholi. Vaa nguo za kujikinga kama vile aproni, miwani, kinyago, glavu na viatu. Tumia njia mwafaka za kutupa uchafu (kuzika au kuchoma). Tumia mchanganyiko wa klorini ya 0.5% kwa dakika 10 kusugua, kuondoa vimelea au kutakasa vifaa vya chuma au glasi. Kisha safisha vifaa kwa maji moto na yenye sabuni au utumie mashine ya kutakasa.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.5 (linatathmini Matokeo ya Somo la 3.4)

Unachunguza nini (na ni mara ngapi) ili kuchunguza jinsi leba ya Almaz inavyoendelea.

Answer

Pima ishara muhimu za mwanamke: shinikizo la damu na halijoto baada ya kila saa 4, na mpigo wa mshipa baada ya kila dakika 30.

Chunguza marudio, urefu na uthabiti wa mikazo yake baada ya kila dakika 30. Mikazo hutokea kila mara, kali na ya haraka leba yake inapoendelea kukua.

Chunguza uke wa mwanamke mjamzito baada ya kila masaa 4 ili kutathmini upanuzi wa seviksi . kiwango cha kawaida cha kupanuka kwa seviksi ni angalau senitmita 1 kwa saa 1 katika leba.

Chunguza kushuka kwa sehemu tangulizi baada ya saa 2. Gusa fumbatio ili huhisi kichwa cha fetasi ukilinganisha na ukingo wa pelvisi, au uchunguze uke.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.6 (linatathmini Matokeo ya Somo la 3.4)

Ni ishara gani inayoonyesha kuwa mtoto ana ufadhaiko?

Answer

Uwepo wa mekoniamu ya rangi ya kijani kibichi katika kiowevu cha amnioni inayotoka ukeni mwa Almaz inaashiria kuwa fetasi iko katika hali ya kufadhaika. Mekoniamu ni kinyesi cha kwanza cha mtoto na kwa kawaida huwa hatoi kinyesi hadi azaliwe. Kima cha mpigo wa moyo wa mtoto anafadhaika wakati wa leba na kuzaliwa kinaweza kuwa juu au chini zaidi ya kiwango cha kawaida cha 100 -180 kwa dakika.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 3.7 (linatathmini Matokeo ya Somo la 3.1, 3.2 na 3.6)

Ni yapi kati ya kauli hizi ambayo si kweli? Katika kila mmojawapo, eleza isiyo sahihi.

  • A.Hiari ya mjamzito inamaanisha uheshimu namna ambavyo mjamzito angependa kuzaa
  • B.Mwanamke hapaswi kunywa chochote iwapo atatapika katika kipindi cha kwanza cha leba.
  • C.Marudio ya mikazo yanaashiria jinsi mikazo ilivyochungu.
  • D.Kutoka kwa mekoniamu ukeni ni ishara kuwa fetasi inafadhaika.
  • E.“Safi tatu” ni: mikono safi, mahali safi (pa kuzalishia) na vifaa safi.

Answer

  • A.Ni kweli. Kuheshimu hiari ya mjamzito inajumuisha namna ambavyo angependa kuzaa.
  • B.Si kweli. Mjamzito anapaswa kunywa angalau kikombe kimoja cha kiowevu baada ya kila saa 1 ili asipoteze maji mwilini, katika kipindi cha kwanza cha leba.
  • C.Si kweli. Marudio ya mikazo inamanisha ni mara ngapi yanakuja kwa muda wa dakika 10 wakati wa leba. Marudio haimaanishi jinsi mikazo ilivyo na uchungu, ambayo ni uthabiti wa mikazo.
  • D.Ni kweli. Mekoniamu inayotoka ukeni ni ishara kuwa fetasi iko katika hali ya ufadhaiko.
  • E.Ni kweli.“Safi tatu” ni: mikono safi, mahali safi (pa kuzalisha) na vifaa safi.

Mwisho wa jibu