4.9 Tathmini hali ya afya ya mama

Wakati wa leba na kuzaa, baada ya utathmini wako kamilifu wa mwanzo, afya ya mama hufuatiwa na upimaji wa ishara muhimu za mama: shinikizo la damu, mpigo wa moyo, joto, na kiasi cha mkojo. Shinikizo la damu hupimwa kila baada ya saa 4. Mpigo wa moyo hunakiliwa baada ya kila dakika 30. Joto, hunakiliwa kila baada saa 2. Kiasi cha mkojo hunakiliwa kila wakati mama akikojoa. Ukitambua mwendeleo wa mabadiliko usio kawaida kwa vipimo hivi vyote, mpe mama rufaa kwa kituo cha afya cha gazi ya juu.

4.8.4 Amnioni kama dalili ya tatizo la fetasi

Muhtasari wa Kipindi cha 4