Malengo ya Somola Kipindi cha 4 cha Somo

Baada ya Kipindi hiki cha somo, unaweza:

4.1 Kueleza na kutumia kwa ufasaha maneno yote muhimu yaliyo kwa herufi nzito. (Swali la Kujitathmini 4.1 na 4.3)

4.2 Kuelezea umuhimu na matumizi ya patografu katika ufuatiliaji wa maendeleo ya leba. (Swali la Kujitathmini 4.1 na 4.2)

4.3 Kuelezea sehemu za patografu na muda sahihi wa vipindi vya kuandika uchunguzi wako na vipimo. (Swali la Kujitathmini 4.1 na 4.3)

4.4 Kuelezea viashiria katika patografu vinavyoonyesha maendeleo mazuri ya leba, na dalili ya hali njema ya fetasi pamoja na ya mama. (Swali la Kujitathmini 4.3)

4.5 Kutambua viashiria katika patografu kwa rufaa ya haraka hospitalini wakati wa leba. (Swali la Kujitathmini 4.3)

Kipindi cha 4 cha Somo Tumia Patografu

4.1 Kwa nini patografu ni muhimu