4.6 Tathmini ufinyanzi na utengenezaji wa kaputi

Mchoro 4.4 Mishono na utosi katika fuvu ya mtoto mchanga.

Mifupa tano zisizoungana na fuvu ya fetasi huunganishwa na mishono, ambazo hupindika wakati wa kuzaa. Maeneo mawili yaliyo makubwa na nyororo huitwa utosi (Mchoro 4.4). Msongamano katika mishono na utosi inaruhusu mifupa ya fuvu kupishana ikiwa mikazo inalazimisha kichwa chini kwa njia ya uzazi. Kupishana kwa mifupa ya fuvu ya fetasi huitwa ufinyanzi. Kichwa cha mtoto kinaweza kuonekana kimechongoka au kunyooka wakati anazaliwa (Mchoro 4.5).

Mchoro 4.5 Mabadiliko ya kawaida katika ufinyanzi wa fuvu ya mtoto mchanga, ambayo kwa kawaida hupotea katika siku 1-3 baada ya kuzaliwa.

Baadhi za fuvu ya mtoto huwa na sehemu iliyovimba iitwayo kaputi katika eneo lililokuwa limefinywa kwa seviksi wakati wa leba na kuzaa (Mchoro 4.6). Kaputi huwa kawaida hata wakati wa leba inayoendelea kikawaida. Kaputi ambayo inaendelea katikati ni ya kawaida. Kaputi inayotokezea kwa upande mmoja si ya kawaida. Hisi ukichunguza ufinyanzi au kaputi mtoto anaposonga chini katika njia ya uzazi. Ukigundua mojawapo, hakikisha kwamba ufunguzi wa pelvisi ni mkubwa kutosha mtoto kupitia. Pelvisi ndogo huwa kawaida kwa wanawake waliokuwa wana utapiamlo wakiwa watoto. Pelvisi ndogo ni kisababishi cha mara kwa mara ya leba ya muda mrefu na matatizo.

Mchoro 4.6 Kaputi ya fuvu ya fetasi huwa ya kawaida ikitokea katikati, lakini si kawaida ikitokea upande mmoja.

Uvimbe katika upande mmoja wa kichwa cha mtoto mchanga ni ishara hatari. Mpe mtoto rufaa ya haraka hospitalini. Damu au viowevu vingine vinaweza kukua katika fuvu la mtoto.

4.5 Kushuka kwa kichwa cha fetasi

4.6.1 Kunakili ufinyazi kwenyepatografu