Malengo ya Somo la Kipindi cha 5

Baada ya Kipindi hiki cha somo, utaweza:

5.1 Kueleza na kutumia kwa usahihi maneno muhimu yaliyo kwenye herufi nzito. (Maswali ya kujitathmini 5.1, 5.2 and 5.3)

5.2 Kueleza dalili za hatua ya pili ya leba. Kueleza kitendekacho kwa mama na mtoto ateremkapo chini kuelekea kwenye uke. (Maswali ya kujitathmini 5.1 na 5.2)

5.3 Kueleza jinsi ya kukadiria iwapo hatua ya pili itaendelea katika hali ya kawaida. Kueleza jinsi ya kutambua dalili za kuonya kwamba leba haiendelei ipasavyo.

5.4 Kueleza jinsi ya kutekeleza kuzaliwa kawaida kwa mtoto aliye na afya na kumpatia huduma mara tu azaliwapo.

5.5 Kufafanua jinsi ya kusaidia kujenga uhusiano mwema kati ya mama na mtoto mchanga baada ya kuzaliwa. (Swali la kujitathmini 5.5)

Kipindi cha 5 Tekeleza Uzalishaji wa Kawaida

5.1 Kutambua dalili za hatua ya pili ya leba