5.1 Kutambua dalili za hatua ya pili ya leba

Njia ya kipekee na hakika ya kutambua hatua ya pili ya leba ni kupanuka kabisa kwa seviksi. Njia pekee ya kutambua kuwa seviksi imepanuka kabisa ni kuchunguza uke. Lakini kumbuka urudiaji wa uchunguzi wa uke unaweza kusababisha maambukizi. Ni bora kutochunguza uke zaidi ya mara moja kila masaa 4. Hata hivyo pima upanuzi kabisa katika hali hizi:

  • Unapohesabu mipigo ya moyo ya fetasi na iwe kiwango cha kawaida cha mipigo ya 120-160 kwa dakika).
  • Kuna umwagikaji wa ghafla wa kiowevu cha amnioni ambacho kinadhihirisha hatari ya prolapsi ya kambakitovu au kuachilia kwa plasenta.
  • Utagundua dalili za hatua ya pili ya leba kabla ya wakati uliopangwa kwa uchunguzi wa uke. (Kisanduku 5.1 linaorodhesha dalili za hatua ya pili ya leba)

Ukiwa na tajriba huhitaji uchunguzi wa uke kufahamu wakati mjamzito yuko karibu kusukuma.

Kisanduku 5.1 Dalili za hatua ya pili

Iwapo mama ana dalili mbili au zaidi ya hizi, kuna uwezekano kuwa ana hatua ya pili ya leba:

  • Anahisi uchungu wa kusukuma ambao hawezi kuuzuia (anasema kuwa ni lazima apitishe kinyesi).
  • Anazuia pumzi au mguno wa kujivuta.
  • Anaanza kutoa jasho.
  • Hali yake inabadilika. Anaanza kulala au kuwa na makini zaidi.
  • Viungo vyake vya uzazi vya nje au mkundu huanza kupanuka na maumivu ya misuli.
  • Anahisi kichwa cha mtoto kikianza kusonga kuelekea kwenye uke.

Mstari wa zambarau huonekana katikati ya matako ya mama yatawanyikapo kutokana na msukumo wa kichwa cha mtoto.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 5

5.1.1 Ni nini hutendeka katika hatua ya pili ya leba?