5.1.1 Ni nini hutendeka katika hatua ya pili ya leba?

Katika hatua ya pili, wakati mtoto yuko kwenye uke, viungo vya uzazi vya mama hupanuka kwa kujikaza. Mkundu wake hufunguka kidogo. Katikati ya maumivu ya misuli viungo vya uzazi hupumzika. (Mchoro 5.1)

Mchoro 5.1 Viungo vya uzazi hupumzika katikati ya mikazo

Kila mikazo ya misuli (na kila mama asukumapo) mtoto husonga chini. Katikati ya mikazo, uterasi ya mama hupumzika na kuvuta mtoto juu kidogo. (Mtoto hayuko juu sana kuliko vile alivyokuwa kabla ya mikazo)

Baada ya muda mdogo, utaona kichwa cha mtoto kwa kila mkazo. Mtoto husonga kama wingu la bahari; ndani na nje, lakini kila mara akiwa karibu kuzaliwa. (Vielelezo 5.2a-d)

Mchoro 5.3 Kichwa cha fetasi hunyosha mlango wa uke kwa kiasi cha kiganja chako.

Kichwa cha mtoto kinyooshapo mlango wa uke kwa kiasi cha kiganja chako, kichwa hukaa katika mlango. (Mchoro 5.3) Kichwa kikaapo kwa mlango hata katikati ya mikazo, kichwa kinafanikiwa. Baada ya kichwa kuzaliwa, mwili wote hutoka nje kwa urahisi kwa msukumo mmoja au miwili.

5.1 Kutambua dalili za hatua ya pili ya leba

5.1.2 Mtoto husongaje kupitia kwa njia ya uzazi?