5.2.2 Msaidie mama wakati anaposukuma

Mchoro 5.6 Kwa upole mhimize mama kusukuma anapohisi haja hiyo.

Seviksi ikipanuka kikamilifu, mwili wa mama husukuma mtoto nje. Baadhi ya wahuduma wa afya hupatwa na furaha sana wakati wa hatua ya kusukuma. Wanampigia mama kelele, "Sukuma! Sukuma "! Lakini kina mama kawaida hawahitaji kusaidiwa ili kusukuma. Miili yao husukuma kwa kawaida. Wakati wanahimizwa na kuungwa mkono, mara nyingi wanawake husukuma kwa jinsi sawa na kutoa mtoto nje.

Ikiwa vigumu kwa mama kusukuma, usimkemee au kumtisha. Kamwe usimtusi au kumpiga mama ili kumfanya asukume. Ikiwa mama amekasirika au ana uoga, kuzaa kunaweza kuendelea polepole. Badala yake muelezee jinsi ya kusukuma vizuri ( Mchoro 5.6). Kila mkazo wa uterasi ni nafasi mpya. Msifu kwa kujaribu.

Mwambie mama unapoona sehemu zake za siri zinapotokezea nje. Mueleze kwamba mtoto anasonga chini. Utakapoona kichwa, uliza mama aiguse. Anaweza kusukuma bora zaidi.

Mwache mama achague upande anahisi ndio nzuri kwake. Ulijifunza kuhusu pande mbalimbali katika kipindi cha kwanza katika Kipindi cha 3 cha Somo. Kumbuka kwamba si vizuri kwa mama kulala chali katika uzaaji wa kawaida. Iwapo analala chali, mishipa inayopelekea mama na mtoto damu hufinywa. Uzaaji unaweza kuendelea polepole.

Mchoro 5.7 Hali tofauti tofauti katika hatua ya pili ya leba.

5.2.1 Angalia mpigo wa moyo wa mtoto

Tazama dalili za hatari