Tazama dalili za hatari

Usisukume uterasi chini ili kusaidia mama kusukuma mtoto. Kusukuma uterasi kunaweza kusababisha plasenta kutengana au kupasuka kwenye uterasi.

Tazama mwendo wa kila uzalishaji. Iwapo uzalishaji utachukua muda mrefu mno, mpeleke mama hospitalini. Mpeleke mama hospitalini ili kuzuia matatizo makubwa au hata kifo akiwa katika leba.

Watoto wa kwanza wanaweza kuchukua saa 2 kamili ya mikazo na kusukuma vizuri ili azaliwe. Watoto wa pili na wa baadaye kwa kawaida huchukua chini ya saa 1. Tazama mwendo wa kichwa cha mtoto kinavyosonga chini kwa njia ya uzazi. Katika uzalishaji wa kawaida na ulio na afya, mtoto anaendelea kusonga chini (polepole sana), na mpigo wa moyo wa mtoto ni ya kawaida. Mama ana nguvu ya kutosha. Mhimize mama kusukuma mpaka kichwa kitokee.

Ikiwa mama atasukuma kwa muda mrefu bila maendeleo, matatizo makubwa yanaweza kutokea. Leba ambayo haiendelei inaweza kusababisha fistula, kupasuka kwa uterasi, pia kifo cha mtoto au mama. (Katika Kipindi cha 10, ulijifunza kuhusu kupasuka kwa uterasi.) Viungo vya uzazi vya mama vinapaswa kuvimba baada ya mama kusukuma kwa nguvu kwa dakika 30. Ikiwa viungo vya uzazi havivimbi, au uvimbe mdogo hautazidi, kichwa kinaweza kuwa hakisongi chini. Iwapo mama atasukuma kwa muda wa saa 1 na mtoto hasongi chini, atahitaji usaidizi.

Iwapo kipindi cha leba kitazidi wakati huu bila maendeleo yanayofaa, mpe mama rufaa mara moja:

  • Saa 1 bila maendeleo yanayofaa (multigravida)
  • Saa 2 bila maendeleo yanayofaa (primigravida)

Wakati kipindi cha pili cha leba kinapoendelea vizuri, utaona mabadiliko muhimu pahali pa kichwa cha mtoto. Mpe mama rufaa ya hospitali au kituo cha afya mara moja ukiona dalili hizi:

  • Mama yuko katika kipindi cha pili cha leba, lakini mtoto hajashuka.
  • Kaputi au ufinyanzi wa fuvu uliozidi kutokea kwa mtoto.

5.2.2 Msaidie mama wakati anaposukuma

5.3 Tekeleza uzalishaji wa mtoto