5.3.2 Toa kichwa cha mtoto wakati anapozaliwa

Mchoro 5.8 Msaidie kutoa kichwa cha mtoto.

Nawa mikono vizuri na uvae glavu safi na vifaa vingine vya kukinga vimelea.

Safisha eneo la msamba kwa kutumia antiseptiki na uweke nguo safi juu ya mapaja ya mama.

Finya msamba kwa kutumia mkono mmoja kwa uthabiti. (Msamba ni ngozi iliyo kati ya ufa wa uke na mkundu.) Mkono huu huweka kidevu cha mtoto karibu na kifua chake. Katika mtindo huu, kichwa hutoka kwa urahisi (Mchoro 5.8). Funika mkundu wa mama na kipande cha nguo. Mara kwa mara mama husukuma kinyesi (mavi) anaposukuma mtoto.

Kwa utaratibu, tumia mkono wako mwingine kufinya kichwa cha mtoto kiteremke chini. Kufinya huku kwa utaratibu, huweka kichwa cha mtoto kiiname chini.

Baada ya kichwa kutokea ukeni, uso hujitokeza kwenye msamba.

Safisha pua na kinywa cha mtoto. Inaweza kubidi usafishe pua na kinywa cha mtoto kabla ya mwili wote kutoka ili aweze kupumua. Ikiwa mtoto ana kamasi au maji kwa pua au kinywa chake, funga kidole kwa kitambaa safi na uyapanguze kwa utaratibu.

5.3.1 Zuia kuraruka kwa ufa wa uke

5.3.3 Angalia kama kambakitovu iko shingoni mwa mtoto