5.3.6 Kata kambakitovu

Kawaida huhitajiki kukata kambakitovu mara moja. Iwache ikiwa imeshikilia ili kumsaidia mtoto kumpatia madini ya iron ya kutosha katika damu yake. Baadhi ya damu hutoka kwa plasenta kupitia kambakitovu hadi kwa mtoto. Unaposubiri kukata kambakitovu, lazima mtoto akae juu ya fumbatio ya mama, ambapo ndipo pahali pazuri zaidi kwa mtoto. Subiri hadi kambakitovu iache kudunda na ionekana kama ikiwa tupu.

Hata hivyo, ikiwa mama ana maambukizi ya VVU au hali yake haijulikani, kata kambakitovu mara tu baada ya kukauka na kupata joto.

Mchoro 5.11 Kata kambakitovu.

Tumia uzi au klampu safi kufunga kwa nguvu au uweke klampu kwa kambakitovu kwa upana wa vidole viwili kutoka fumbatio ya mtoto. (Hatari ya mtoto kupata maambukizi ya pepopunda ni makubwa wakati kambakitovu imekatwa mbali na mwili.) Funga fundo la mraba (Mchoro 5.11).

Weka uzi nyingine safi au klampu kwa upana wa kidole kimoja mbali na fundo la kwanza. Iwapo huna klampu kwenye kambakitovu karibu na mama, ongezea fundo la tatu vidole viwili kutoka kwa fundo la pili. Kuweka fundo mara mbili kwa kambakitovu hupunguza hatari ya kutokwa na damu.

Tumia makasi au wembe safi kukata kambakitovu baada ya fundo la pili. (Kwa mfano, fundo la kwanza liko sentimita 3 kutoka fumbatio la mtoto na la pili liko kwa umbali wa sentimita 5.)

5.3.5 Kuzalisha mwili wa mtoto

5.4 Huduma ya mtoto baada ya kuzaliwa