5.4.1 Kuzuia maambukizi na utunzaji wa kambakitovu

Ili kuzuia maambukizi kwa mama na mtoto, fuata hatua hizi:

  • Nawa mikono yako.
  • Safisha msamba wa mama.
  • Usiweke vitu visivyo safi katika uke.
  • Safisha pahali pa kuzalia.
  • Tumia vifaa safi kufunga na kukata kambakitovu.

Weka gutu ya kambakitovu safi na iliyokauka ili kuzuia maambukizi. Safisha tu kwa sabuni na maji safi iwapo imechafuka. Kumbuka:

  • Usifunike au kuweka kitu chochote.
  • Kama kambakitovu inavuja damu, ifunge tena.

Gutu kwa kawaida huanguka siku 4-7 baada ya kuzaa. Wakati gutu bado imeshikilia, iweke nje ya napi na mbali na mkojo na kinyesi.

Usiweke uchafu au kinyesi cha mnyama kwenye gutu la kambakitovu! Uchafu au kinyesi cha mnyama hazilindi gutu, bali husababisha maambukizi hatari.

5.4 Huduma ya mtoto baada ya kuzaliwa

5.4.2 Kagua mtoto