Muhtasari wa Kipindi cha 5

Katika Kipindi cha 5, ulijifunza mambo haya:

  1. Hatua ya pili ya leba inaanza wakati seviksi imepanuka kabisa na huisha wakati mtoto amezaliwa. Toa uzingatiaji wa karibu, huduma yenye ujuzi, na hatua ya haraka kwa uzalishaji salama, safi.
  2. Dalili hizi zinaonyesha hatua ya pili ya leba: mama anahisi hamu isiyozuilika ya kusukuma na anashikilia pumzi yake au kupumua kwa nguvu wakati wa mikazo. Mama anaanza kutoa jasho na hali ya sununu yake inageuka. Viungo vya uzazi vya nje au mkundu wa mama hujitokeza nje wakati wa mikazo. Mama anahisi kichwa cha mtoto kikisongea kwenye uke. Mstari wa zambarau unajitokeza katikati ya makalio ya mama.
  3. Angalia dalili muhimu za mama. Angalia mpigo wa moyo wa fetasi na kiwango cha uteremkaji wa kichwa cha mtoto. Angalia mara kwa mara ili kuhakikisha kwamba leba inaendelea kwa kawaida.
  4. Chunguza dalili za hatari ya kuwa leba haiendelei na umpe mama rufa.
  5. Msaidie mama wakati anasukuma na kuzaa mtoto.
  6. Ikiwa kambakitovu imezungushwa shingoni mwa mtoto, ikate kabla ya mwili kuzaliwa. Halafu hakikisha kwamba mama anasukuma kwa nguvu ili mtoto atoke nje haraka.
  7. Dumisha usafi wakati wote wa leba na wa kuzaa. Usafi huzuia maambukizi kwa mama na mtoto.
  8. Mpatie mtoto mchanga joto na uhakikishe kuwa anapumua vizuri.
  9. Anzisha unyonyeshaji wa mapema.

5.4.4 Unyonyeshaji wa mapema

Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 5