Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 5

Sasa kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki cha somo, jibu maswali haya kutathmini ulichojifunza. Angalia majibu yako na nakala juu ya Maswali ya kujitathmini hapo mwisho.

Maswali ya kujitathmini 5.1 (Malengo ya Somo la 5.1, 5.2, na 5.3)

Ni maelezo gani ambayo si kweli? Katika kila hali, eleza ni lipi lisilo sahihi.

  • A.Upanuzi kamili wa seviksi hadi sentimita 10 ndio ishara muhimu zaidi kwamba hatua ya pili ya leba imeanza.
  • B.Katika hatua ya pili, sehemu za siri za mama hutokea wakati wa mikazo na hupungua katikati ya mikazo.
  • C.Kujichomozani wakati kichwa cha mtoto huzaliwa kabisa.
  • D.Katika uzaaji wa kawaida, mtoto huteremka kwenye njia ya uzazi akiangalia upande wa mbele wa mwili wa mama. Mgongo wa mtoto ukiangalia upande wa uti wa mama
  • E.Wakati mtoto yuko katika njia ya uzazi, Mpigo wa moyo huongezeka wakati wa mkazo.
  • F.Katika hatua ya pili ya leba, mruhusu mama kuchagua ni upande gani ule anahisi angependelea kukaa wakati anapopata hisi ya kusukuma.

Answer

  • A.ni kweli. Upanuzi kamili wa seviksi hadi sentimita 10 ndio ishara muhimu zaidi kwamba hatua ya pili ya leba imeanza.
  • B.ni kweli. Katika hatua ya pili, viungo vya uzazi vya mama hutokea wakati wa mikazo na hupungua katikati ya mikazo.
  • C.si kweli. Kujichomoza ni wakati kichwa cha mtoto hupanua ufunguzi wa uke hadi ukubwa wa kiganja chako. Kichwa hukaa katika ufunguzi hata kati ya mikazo.
  • D.si kweli. Katika uzaaji wa kawaida, mtoto huteremka kwenye njia ya uzazi na huangalia nyuma ya mwili wa mama. Mgongo wa mtoto huangalia upande wa fumbatio yake.
  • E.si kweli. Wakati mtoto akiwa katika njia ya uzazi, mpigo wa moyo wa fetasi huenda chini (sio haraka) ikiwa na mkazo.
  • F.ni kweli. Katika hatua ya pili ya leba, mruhusu mama kuchagua ni upande gani ule anahisi angependelea kukaa wakati anapopata haja ya kusukuma.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 5.2 (Malengo ya Somo la 5.3)

Orodhesha dalili 4 za kuonyesha kuwa hatua ya pili ya leba haiendelei kwa njia ya kawaida.

Answer

Dalili za kuonyesha kwamba hatua ya pili haiendelei kawaida ni pamoja na hizi:

  • Mpigo wa moyo wa fetasi inakaa zaidi au chini ya kiwango cha kawaida (midundo 120-160 kwa dakika) hata kati ya mikazo.
  • Amnioni Kutoka kwa ghafla ukeni, ambayo inaweza kuonyesha hutokaji wa kambakitovu au kuachilia kwa plasenta.
  • Mama aliye Multigravida anasukuma kwa saa 1 na mtoto hajateremka kwa njia ya uzazi. Au mama aliye primigravida anasukuma kwa saa 2 na hakuna maendeleo mazuri.
  • Mtoto hateremki na ukuaji wa kaputiau ufinyanzi mwingi wa fuvu ya fetasi.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 5.3 (Malengo ya Somo la 5.4)

Fikiria kwamba kichwa cha mtoto kimezaliwa. Subiri mkazo ujao ili kutoa mabega ya mtoto wakati wa uzalishaji. Unapaswa kufanya nini ikiwa kambakitovu imezunguka shingo ya mtoto?

Answer

Kwanza, jaribu kulegeza kambakitovu na uipitishe juu ya kichwa cha mtoto. Iwapo huwezi kuilegeza na inazuia mtoto kutoka, weka klampu kwa kambakitovu katika maeneo mawili. (Au ifunge na uzi iliyofishwa vimelea.) Kata kambakitovu katikati ya klampu. Usimkate mama au shingo ya mtoto.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 5.4 (Malengo ya Somo la 5.4 na 5.5)

Panga upya hatua hizi katika mpangilio sahihi wa uzalishaji wa mtoto na mara tu baadaye.

  • A.Baada ya kichwa cha mtoto kutolewa wakati wa kuzaa, panguza pua na kinywa ili kumsaidia kupumua.
  • B.Nawa mikono yako vizuri na uvae glavu safi na mavazi mengine ya kujikinga.
  • C.Ili kuzuia kuraruka kwa msamba wa mama, toa mabega ya mtoto mmoja kwa wakati.
  • D.Finya msamba wa mama kwa nguvu na mkono mmoja.
  • E.Wakati mtoto amezaliwa, mweke juu ya fambatio ya mama na umpanguze na nguo safi.
  • F.Safisha sehemu ya msamba wa mama kwa antiseptiki.
  • G.Weka klampu au funga kambakitovu katika maeneo mawili na ukate katikati ya hizo klampu.
  • H.Tumia mkono wako mwingine polepole kuweka pumzi ya kueleka juu ya kichwa cha mtoto ili kujipinda chini.
  • I.Funika mtoto ili kumpatia joto na umnyonyeshe mara moja.
  • J.Tumia kipande cha nguo au shashi kufunika mkundu wa mama ikiwa kinyesi chochote kitatoka nje wakati anaposukuma.
  • K.Chunguza kama kambakitovu haijazunguka shingo ya mtoto.

Answer

Mpangilio huu ndio sahihi:

  • B Nawa mikono yako vizuri na uvae glavu safi na mavazi mengine ya kujikinga.
  • F Safisha sehemu ya msamba wa mama na antiseptiki.
  • D Bana msamba wa mama kwa nguvu na mkono mmoja.
  • J Tumia kipande cha nguo au shashi kufunika mkundu wa mama ikiwa kinyesi chochote kitatoka nje wakati anaposukuma.
  • H Tumia mkono wako mwingine kuweka polepole pumzi ya kuelekea juu ya kichwa cha mtoto kwelekea chini ili kujipinda chini. A Baada ya kichwa cha mtoto kuzaliwa, mpanguze pua na kinywa ili kumzaidia kupumua.
  • K Chunguza kama kambakitovu haijazunguka shingo ya mtoto.
  • C Ili kuzuia kuraruka kwa msamba wa mama, toa mabega ya mtoto mmoja kwa wakati.
  • E Wakati mtoto amezaliwa, mweke juu ya fambatio ya mama na umpanguze kwa nguo safi.
  • I Funika mtoto ili kumweka joto na humnyonyeshe mara moja.
  • G Weka klampu au funga kambakitovu katika maeneo mawili na ukate katikati ya hizo klampu.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 5.5 (Malengo ya Somo 5.5)

Ni kwa jinsi gani unaweza kuhamasisha mama na mtoto wake kujuana?

Answer

Ili kusaidia mama na mtoto wake kujuana, weka mtoto haraka juu ya fumbatio ya mama mara tu anapozaliwa. Mnyonyeshe mapema. Usitenganishe mama na mtoto wake katika saa la kwanza baada ya kuzaliwa.

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 5