Malengo ya Masomo ya Kipindi cha 7

Baada ya Kipindi hiki cha somo, utaweza:

7.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyo katika herufi nzito. (Swali la kujitathmini 7.2)

7.2 Kutoa kwa muhtasari dalili za asifiksia ya watoto wachanga zinazoashiria kuwa unapaswa kuanza uhaishaji (uhaisho) wa mtoto mchanga. (Swali la kujitathmini 7.1)

7.3 Kueleza jinsi ya kutumia mbinu za wastani za uhaisho kuwasaidia watoto wachanga kupumua. (Maswali ya kujitathmini 7.1 na 7.2)

7.4 Kutambua vifaa unavyopaswa kuwa navyo ili kumhaisha mtoto mchanga na jinsi ya kuvitumia ifaavyo. (Swali la kujitathmini 7.3)

7.5 Kueleza vitu usivyotakiwa kufanya unapomtathmini mtoto kwa matatizo ya kupumua. (Swali la kujitathmini 7.4)

7.6 Kutoa muhtasari wa hatari kuu za kiafya na huduma muhimu kwa watoto wachanga. (Swali la kujitathmini 7.5)

Kipindi cha 7 cha somo Uhaishaji wa mtoto mchanga

7.1 Upumuaji na uhaishaji wa mtoto mchanga