7.1.1 Jinsi mtoto mchanga mwenye afya anavyopumua

Kwa kawaida, mtoto mwenye afya hupumua mwenyewe mara tu baada ya kuzaliwa (Picha 7.1). Iwapo kupumua kulianza kwenyewe na mtoto anapumua bila kusaidiwa, mambo haya ni kweli:

  • Fetasi haikupata asifiksia ilipokuwa kwenye uterasi.
  • Mfumo wa kupumua unafanya kazi vizuri.
  • Mfumo wa moyo na mishipa ya damu unafanya kazi vizuri.
  • Ubongo unaratibu mizunguko inayohitajika kwa mfululizo wa upumuaji bora. (Ubongo unafanya kazi vizuri.)
Picha 7.1 Mtoto mchanga aliyezaliwa baada ya kutimiza muda kamili wa ujauzito na anayepumua vizuri ana ngozi yenye rangi ya waridi na mikono na miguu iliyokunjwa kiasi. Amebadilika vyema kutoka kwa uterasi ya mama hadi nje. (Picha: Dr Mulualem Gessese)
  • Je, unachunguza vipi hali njema ya mtoto wakati wa leba na kuzaa?

  • Fetasi yenye afya ina midundo ya moyo kati ya 120 na 160 kwa dakika. Membreni za fetasi zinapopasuka, kiowevu cha amnioni kinachovuja kutoka ukeni mwa mama huyo ni angavu. Kiowevu hakina rangi nyekundu ya damu au rangi ya kijani au nyeusi ya mekoniamu. (Mekoniamu ni kinyesi cha kwanza cha mtoto.)

    Mwisho wa jibu.

Umechunguza mdundo wa moyo wa fetasi mara kwa mara katika kipindi chote cha leba. Uliyaandika matokeo kwenye patografu jinsi ulivyojifunza katika Kipindi cha 4 cha somo. Ulimpa mama rufaa iwapo mtoto ambaye hajazaliwa alionyesha dalili za kuathirika. Kwa hivyo, usishughulikie uzazi wa mtoto aliye na asifiksia. Hata hivyo, matatizo katika uzazi yanaweza kutokea bila kutarajiwa au unaweza kuitwa kumhudumia mwanamke aliye katika kipindi cha pili cha leba. Kwa hivyo, ni lazima ujue jinsi ya kumhaisha mtoto mchanga iwapo utashughulikia uzazi wa mtotot aliye na asifiksia.

7.1 Upumuaji na uhaishaji wa mtoto mchanga

7.1.2 Asifiksia ya mtoto mchanga